Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Afya cha Nanyumbu?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY Y. MHATA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu haya ya Serikali, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kituo hiki ninachokieleza ni cha muda mrefu sana. Cha kushangaza kituo hiki kililetewa vifaa, vifaa tiba, vyote vya kituo cha afya ambapo kituo cha afya hakijajengwa. Sasa nauliza vile vifaa walivyovileta walikuwa na malengo gani, yaani vitumike wapi wakati kituo hakijafanyiwa ukarabati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; vifaa vile sasa hivi vimepelekwa katika sehemu nyingine je, Waziri anawahakikishia vipi wananchi wa ile Tarafa kwamba endapo watafanya ukarabati vifaa vile vitarejeshwa pale? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mhata kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, la kwanza kuhusu hiki kituo cha muda mrefu ambacho kimepelekewa vifaatiba, ni wao wenyewe kama halmashauri ambao wanapanga vifaatiba viende kwenye kituo gani cha afya. Kwa hiyo ina maana wao walifanya maamuzi ya kupeleka vifaatiba hivi vipya katika kituo ambacho ni chakavu.

Mheshimiwa Spika, nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nanyumbu kutenga fedha kwa ajili ya kuanza kukarabati Kituo hiki cha Afya kongwe cha Nanyumbu wakati bado tunatafuta fedha. Nitakaa na Mheshimiwa Mhata kuona ni namna gani tunaweza tukapata fedha ya kupeleka kukarabati kituo hiki cha afya.

Mheshuimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la vifaa hivi tiba ambavyo vimehamishwa kwenda kwenye Kituo cha Afya cha Tarafa nyingine na kuhama hapa Nanyumbu. Katika mwaka wa fedha wa 2023/2024, Serikali imetenga bajeti ya bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba. Ni jitihada kubwa ya mama yetu Samia Suluhu Hassani, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha kwamba tunapata vifaatiba kuanzia ngazi ya zahanati mpaka vituo vya afya. Nimhakikishie Mheshimiwa Mhata kwamba tutapeleka tena vifaatiba vingine katika Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati katika Kituo cha Afya cha Nanyumbu?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua Kituo cha Afya Tandale katika Wilaya ya Kinondoni ili kipate Jengo la Mama na Mtoto na hasa ukiangalia idadi ya watu wanaoishi katika Kata ya Tandale ni wengi sana? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MIKOA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutatuma timu katika kituo hiki cha afya ambacho amekitaja Mheshimiwa Kisangi kufanya tathmini na kuona ukubwa wa eneo uliopo na kama linaweza likahimili kupata majengo mengine. Baada ya tathmini hiyo kufanyika itawasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya kukipanua kituo hiki cha afya.