Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara ya Mjele – Ikuwa hadi Mlima Njiwa kuwa ya Mkoa?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naishukuru Serikali vilevile kwa vile Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi amesharidhia hii barabara sasa hivi kuhudumiwa na TANROADS, lakini iko kwenye hali mbaya sana. Sasa je, ni lini barabara hii itaanza ujenzi ili irekebishwe kuanzia Mjele, Ikukwa na siyo Ikuwa mpaka Mlima Njiwa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika hali hiyo ya barabara, barabara ya Haporoto – Ileya – Ishinda ambayo inahudumia wachimbaji wa Migodi ya Ileya na Ishinda, ni lini barabara hii itapata matengenezo kwa vile nayo iko kwenye hali mbaya sana? Nashukuru. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Njeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema, baada ya kupandishwa hadhi hiyo barabara, TANROADS itaanza utekelezaji kwa bajeti ambayo tunaanza kuitekeleza kwa 2023/2024. Kwa hiyo kwa sasa wenzetu wa TARURA baada ya Juni watatukabidhi na sisi tutaanza utekelezaji huo kwa bajeti mpya, ahsante. (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa kuongezea tu kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi, barabara hii wakati bado ipo kwa TARURA ilikuwa imetengewa shilingi milioni 500 na Road Board kwa ajili ya matengenezo yake. Sasa baada ya kupandishwa hadhi fedha ile itahamia kwa wenzetu wa TANROADS ambapo bado watatekeleza kwenye barabara hii hii shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuijenga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili ya Barabara ya Haporoto – Ileya – Ishinda. Barabara hii ina urefu wa kilometa tisa na kweli nikiri kwamba kwa sasa hali yake si nzuri sana. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 ambao tunauanza mwezi unaofuata, tayari barabara hii imetengewa shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuweza kutengeneza yale maeneo korofi kwa kumwaga changarawe na kuhakikisha kwamba inapitika vizuri, kwa sababu inaelekea katika eneo ambalo lina machimbo. Kwa hiyo nimtoe hofu Mheshimiwa Njeza, kwamba muda si mrefu ataona utekelezaji wa matengenezo ya barabara hii kwa hizi kilometa tisa.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara ya Mjele – Ikuwa hadi Mlima Njiwa kuwa ya Mkoa?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nataka nijue Serikali ina mpango gani wa kupandisha hadhi Barabara ya Bukama - Nyamagaro mpaka Kiangasaga kuwa hadhi ya barabara ya Mkoa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chege kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007, Kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya mwaka 2009 imeelezea wazi namna ya kuomba kupandisha hadhi barabara. Inatakiwa waanze kukaa vikao vyao kule na kupendekeza kwa Kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, Mkoa wao wa Mara. Wakishapendekeza pale, baada ya hapo wanawasilisha maombi yale kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi mwenye dhamana ya ujenzi.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara ya Mjele – Ikuwa hadi Mlima Njiwa kuwa ya Mkoa?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Barabara ya Kibaoni – Endabash itapandisha kuwa hadhi ya Mkoa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyotoka kusema hapo awali, kwa mujibu wa Sheria ile ya Barabara Na. 13 ya mwaka 2007, kifungu cha 11 na Kanuni za Usimamizi wa Barabara ya Mwaka 2009, zinaelezea ule utaratibu, inatakiwa mchakato uanze kwao wenyewe kwa kupendekeza barabara hiyo kupandishwa hadhi kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa, kisha aandikiwe Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi mwenye dhamana ya barabara na atume timu kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa barabara hiyo, ndipo barabara hiyo iweze kupendekezwa na kufikiriwa kupandishwa hadhi.