Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa Mipango na Bajeti zinazopitishwa?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na kusuasua kwa utekelezaji wa bajeti kadri tunavyotenga kwenye Bunge hili kipindi cha bajeti, wakati mwingine kuchelewa kufika au kufika kwa asilimia ndogo. Sasa naomba kufahamu mkakati wa Serikali kutatua changamoto hii, kwa sababu tukitenga bajeti tunatarajia ifike kama tunavyotenga.

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Natamani kufahamu mpaka sasa hivi Serikali imechukua hatua gani kwa Watendaji ambao wamekuwa siyo waaminifu na wabadhilifu wa mali za umma hususan bajeti kadri tunavyotenga badala ya kusubiri taarifa ya CAG pamoja na Mwenge? Ahsante.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nusrat Hanje, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutoa fedha kama zilivyotengwa katika bajeti kadri ya fedha zinavyopatikana. Kwa kuwa, mfumo wetu wa bajeti ni cash budget, pesa zitakusanywa ili ziweze kutumika katika bajeti, hivyo Serikali itaendele kukusanya na kuongeza uwezo wa ukusanyaji wa mapato ili tuweze kutekeleza bajeti kama ilivyopangwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili. Serikali imechukua hatua mbalimbali kwa wale watumishi ambao siyo waadilifu. Hatua hizo ni pamoja na kuwafikisha Mahakamani, wako wale ambao wamefungwa sasa, wako ambao wamesimamishwa kazi na wako ambao wamefukuzwa kazi. Ahsante. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa Mipango na Bajeti zinazopitishwa?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali sasa haioni kuwa ni wakati muafaka wa kukitumia kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kuweza kufatilia bajeti?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inakitumia ipasavyo kitengo hiki cha Ukaguzi wa Ndani na tumekiongezea uwezo mwaka huu uliopita na mwaka ujao tumetenga kuongeza uwezo wa kufanya ukaguzi unaostahiki.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa Mipango na Bajeti zinazopitishwa?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Moja ya eneo ambalo Serikali inatekeleza chini ya asilimia 50 kwenye bajeti na mpango ni ahadi za Viongozi wa Kitaifa.

Je, ni upi mkakati wa Serikali kumaliza ahadi zote za Viongozi wa Kitaifa za miaka ya nyuma? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuimarisha mawasiliano lakini inaendelea kuimarisha makusanyo ya fedha, na hivi nimuombe Mheshimiwa Mbunge naye awe ni Balozi wa kushawishi na kuwashauri wafanyabiashara pamoja na yeye na mimi kuendelea kukusanya kodi ili tuweze kutekeleza ahadi za viongozi wetu kwa wakati.