Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Mbuguni kuanzia Tengeru Sokoni, Arumeru hadi Mererani utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara hii inaunganisha Mikoa miwili, Arusha na Manyara pia ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa. Sasa barabara hii kwa unyeti wake iko busy na imekuwa ni changamoto kubwa sana ya afya kwa wanachi walioko katika barabara hii kwa sababu ya vumbi. Naomba commitment ya Serikali kwamba; Je, ni lini ujenzi utaanza kwa sababu kuna fedha nyingi, kuna mpango wa RISE, kuna Agri - connect. Je, Serikali haiwezi ikafanya utaratibu barabara hiyo ianze kujengwa mara moja baada ya usanifu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna ahadi nyingi sana za Serikali, Viongozi Wakuu za ujenzi wa barabara kwa viwango vya lami, na mojawapo ni barabara ya King’ori kutoka Malula hadi Ngarenanyuki. Naomba niulize barabara ya King’ori kutoka Malula hadi Ngarenanyuki lini itajengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu ni ahadi ya Viongozi Wakuu wa Serikali. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, commitment ya Serikali imeshaonekana na ndiyo maana tayari tumeshaanza taratibu za kujenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami tukitambua kwamba inaenda kwenye sehemu muhimu sana ya kiuchumi eneo la mgodi wa Mererani lakini pia inaunganisha kama alivyosema Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Manyara. Isingekuwa rahisi kufanya chochote kabla ya kukamilisha usanifu. Kwa hiyo, kama fedha inaweza ikatokea yoyote katika kipindi hicho tutafanya, vinginevyo ni kwamba baada ya kukamilisha usanifu basi tutaipangia bajeti kwa mwaka ujao wa bajeti kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu hii barabara aliyoitaja. Ni kweli barabara ya King’ori – Ngarenanyuki ilikuwa inatengenezwa na wenzetu wa TARURA tumekasimiwa, kwa hiyo tunaendelea kutafuta fedha ili tuweze kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami kwa sababu inapita kwenye maeneo makubwa sana ya uzalishaji wa wenzetu ambao ndiyo wanalisha Mji wa Arusha. Ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Mbuguni kuanzia Tengeru Sokoni, Arumeru hadi Mererani utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mpango wa Serikali ni kuunganisha kwa kiwango cha lami kutoka Wilaya kwenda Mkoa. Waziri ni lini Serikali itaanza kujenga barabara Halmashauri ya Wilaya Mbogwe kwenda Geita Makao Makuu ya Mkoa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maganga Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli huo ndiyo mpango na bahati nzuri barabara alizozitaja Mheshimiwa Mbunge zitafadhiliwa na wenzetu wa World Bank kupitia mradi wa RISE ambao sasa hivi wanakamilisha kufanya review ya usanifu wa barabara za kuiunganisha Wilaya ya Mbogwe na Wilaya ya Geita kwa kiwango cha lami. Tunategemea kuanzia mwaka ujao wa fedha kwa sababu taratibu zinaendelea na ni fedha za World Bank, mara baada ya kukamilisha hizo taaratibu ujenzi utaanza kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Mbuguni kuanzia Tengeru Sokoni, Arumeru hadi Mererani utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwanza ninaishukuru Serikali kwa kusaini mkataba wa Barabara ya Sengerema kwenda Nyehunge klilomita 54 lakini awali barabara ile ilisomeka Sengerema - Nyehunge na kipande cha Kahunda kilometa 32. Kilometa 32 za Nyehunge - Kahunda zimeondolewa.

Je, Serikali inaweza kutoa commitment ya kwamba kilometa 32 za Nyehunge - Kahunda pamoja na kipande cha Bukokwa – Nyakalilo zitajengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la, Mheshimiwa Mbunge Shigongo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii katika design, ili - design – wa kilometa zote mpaka hizo kilometa 32 kwenda Kahunda. Lakini tumeanza kuzijenga kulingana na upatikanaji wa bajeti na ndiyo maana commitment ya Serikali tayari tumeshasaini kipande hicho cha kilometa kuanzia Sengerema hadi Nyehunge kwa kuanzia na tukitegemea kwamba pengine katika mwaka wa fedha ujao, basi tutakamilisha hizo kilometa zote zilizobaki kwa sababu ndiyo mapango wa Serikali kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Mbuguni kuanzia Tengeru Sokoni, Arumeru hadi Mererani utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Sengerema - Buchosa inaunganisha na Mkoa wa Geita kipande kidogo tu cha kilometa 14 kutoka Nyehunge kwenda Nzela, Serikali imeishia Nyehunge.

Je, Serikali ina mapango gani kuunganisha kutoka Nyehunge kwenda Nzela ambako Mheshimiwa Waziri unapita?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba tuna kila sababu ya kuunganisha Mkoa na Mkoa. Bahati nzuri hiyo barabara mimi nimeipita, kama nilivyosema kwamba mpango wa Serikali ni kuziunganisha Mkoa na Mkoa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, kadri fedha itakavyopatikana barabara hii ya kutoka Nyehunge hadi Nzela kipande kilichobaki pia kitajengwa kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na Nzela hadi Kome ambayo iko kwenye hatua za manunuzi. Ahsante. (Makofi)