Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES M. MARWA aliuliza:- Je, Serikali imewatafutia eneo mbadala wananchi wa Vijiji vya Kata ya Nyantwari – Bunda wanaofanyiwa uthamini kupitia uhifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa wananchi waliambiwa kwamba watalipwa kwa ekari moja shilingi milioni mbili, kutokana na uhalisia wa maisha, maisha yamepanda juu sana, wananchi waliomba waongezewe kutoka milioni mbili kulipwa shilingi milioni sita. Je, nini tamko la Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mbili, kwa kuwa Kata ile ya Nywatwari kuna wavuvi na wafugaji, je, wafugaji wamekwisha tafutiwa maeneo kwa ajili ya mifugo yao na wavuvi wataangaliwa vipi kwa ajili ya maeneo rafiki ya kuendeleza uvuvi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Agnes na kumpongeza kwa namna ambavyo anaendelea kutetea Wananchi wa Mkoa wa Mara akiwa kama Mbunge wa Mkoa wa Mara. Hili suala la stahili ya hawa wanaopaswa kuhama linafanyika kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo ambapo Wizara ya Ardhi wamekuwa wakifanya uthamini na miongozo yote wanaitumia ili kuhakikisha kwamba suala hili linaendana sambamba na sheria na taratibu na kanuni zilizopo. Endapo kutakuwa na uhitaji wa kuangalia uthamani au namna ya kuongezewa basi tutakaa na Wizara ya Ardhi ili tuweze kujadili kama kuna uwezekano huo.

Mheshimiwa Spika, kwenye hili la pili la wafugaji na wavuvi, kwenye upande wa kuwahamisha tayari uthamini umefanyika ikiwemo mifugo yao, ardhi yao waliyokuwa wanaitumia. Kwa hiyo, watakapokuwa wameenda kwenye makazi mapya yatazingatiwa hayo ikiwemo kutengewa maeneo ya mifugo lakini kwenye suala hili la uvuvi sheria za uhifadhi zitaongozwa kwa sababu maeneo ambayo tunaenda kuyatwaa mengi tutakuwa tunayahifadhi. Kwa hiyo tutaangalia utaratibu unasemaje ili tuweze kukaa pamoja na wavuvi waweze kuangaliwa. (Makofi)