Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa miundombinu ya maji iliyochakaa na kusababisha upungufu wa maji – Chemba?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, mwaka 2018, Serikali ilichimba kisima kwenye Kijiji cha Mayi lakini mpaka leo hakijaweka miundombinu na hivyo hakitumiki, nini kauli ya Serikali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, mwaka wa 2021/2022 Serikali ilitangaza kandarasi ya visima 13, mpaka leo imechimba vitatu tu na hivyo tunawadanganya wananchi. Naomba kujua Waziri anasema nini juu ya visima hivyo ambavyo havijachimbwa? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Monni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kisima kilichochimbwa mwaka 2018, Mheshimiwa Mbunge tutakisimamia kuhakikisha tunaleta usambazaji kwa wanufaika wote kwenye kile kisima. Kwa visima hivi ambavyo tulivipitisha mwaka wa fedha 2022, Mheshimiwa Mbunge Serikali haiwezi kudanganya kwa sababu suala letu sisi ni kuhakikisha tunapeleka huduma kwa wananchi. Kwa hiyo, vile visima vilivyobaki lazima tuvifanyie kazi tutakuja kuvichimba kadiri tunavyopata fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa miundombinu ya maji iliyochakaa na kusababisha upungufu wa maji – Chemba?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini visima vilivyochimbwa katika majimbo ya Ndanda, Nanyumbu na Tandahimba wananchi wake wataanza kuyatumia maji hayo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Agnes Hokororo, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Hokororo naye pia ameshafika ofisini na tumeweza kujadiliana masuala ya visima vyote vilivyochimbwa kwenye haya majimbo aliyoyataja. Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuonane ili tuweze kupanga mkakati baada ya Bunge hili twende kule site tutaangalia namna gani ya kuona tunatekeleza kwa pamoja.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa miundombinu ya maji iliyochakaa na kusababisha upungufu wa maji – Chemba?

Supplementary Question 3

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Sengerema kuna mitambo imewekwa kwa ajili ya kuchimba visima na visima vilivyochimbwa ni vitano kati ya visima 38. Nini kauli ya Serikali kuhusiana na mitambo hiyo kukaa leo mwezi wa pili iko Sengerema na visima havichimbwi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tabasam, Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mitambo hii tumeisambaza mikoa yote na Mkoa wa Mwanza ni mnufaika kwa mitambo ambayo iko Sengerema ilikuwa na michakato inafanyika ili kuona tunaendelea kutenda kazi na nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge mara baada ya Bunge hili kazi zitaendelea na mitambo ile itamaliza visima 38 na kuhamia wilaya nyingine.