Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Kata ya Mjimwema Makambako?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninaomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, shule hii ya Mjimwema Makambako ni shule ambayo Mheshimiwa Mbunge aliiweka moja kati ya vipaumbele vya shule zake ambazo tulivileta TAMISEMI ili ziweza kujengwa kutokana na eneo hili kuwa na uhitaji mkubwa wa sekondari.

Je, ni lini Serikali itafanyia kazi mapendekezo ya Mheshimiwa Mbunge ili shule iweze kujengwa pale?

Swali la pili, hata Wilaya ya Makete nilileta kipaumbele kwenye Kata ya Kigala ambayo kwa muda mrefu haina Shule ya Sekondari ya Kata. Ni lini Serikali itajenga Sekondari ya Kata kwenye Kata ya Kigala ili wananchi waweze kupata elimu kwa mazingira ya karibu? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza. Kuhusu swali hili la kwanza la Kata ya Mjimwema kupata shule, kama nilivyokwisha sema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali kwa sasa ipo mbioni kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya katika Kata ambazo hazina shule kwenye Halmashauri mbalimbali nchini na kila Halmashauri kwenye Halmashauri 184 itapata shule moja. Tumetenga kiasi cha shilingi milioni 570 kwa ajili ya ujenzi wa shule hizo. Awamu ya kwanza ya hizo shule 231 ilienda milioni 470, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeangalia hali ya mabadiliko ya vifaa, bei na kadhalika na kuweka minimum kuwa ni milioni 570. Sasa ni wajibu wa Halmashauri ya Mji wa Makambako wenyewe kuhakikisha kwamba fedha hii inapofika waweke kipaumbele Shule ya Mjimwema ili iweze kujengwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la Kata ya Kigala kule Makete vilevile Halmashauri ya Wilaya ya Makete itapokea shilingi minimum milioni 570 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya katika Halmashauri yao, hivyo basi ni wajibu wao kuhakikisha kwamba wanapeleka fedha katika Kata hii ya Kigala kwa ajili ya ujenzi wa sekondari mpya.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Kata ya Mjimwema Makambako?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye ukarabati wa shule ya Sekondari ya SUA?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Dkt. Ishengoma la Serikali kupeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa shule ya Sekondari ya SUA. Tutatuma timu pale ya Afisa Elimu wetu wa Sekondari katika Halmashauri ile kuweza kufanya tathmini ya nini kinachohitajika kufanyika katika ukarabai ule na watawasilisha taarifa ile Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati wa Shule ya Sekondari SUA.