Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni wananchi kiasi gani wa Wilaya ya Kyerwa wamefikiwa na huduma ya maji safi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, wakati Serikali ikitumia gharama kutafuta vyanzo vya maji, Kyerwa ina vyanzo ambavyo viko tayari; moja ni Mto Kagera lakini na Ziwa Victoria.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza, ni lini Ziwa Victoria na Mto Kagera vitatumika kuwapatia wananchi maji safi na salama ili itimie asilimia 80 kama maeneo mengine?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, wakati Serikali ikiwa na kaulimbiu ya kumtua mama ndoo hata miradi michache iliyopo ya maji wananchi hutembea umbali mrefu kwenda kufuata vyanzo hivyo vya maji.

Swali langu, ni lini au ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha maji hayo yanapatikana kwenye kaya za watu kama ilivyo maeneo ya mjini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anatropia Theonest kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, lini Serikali itatumia Ziwa Victoria? Kwenye bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 Mheshimiwa Waziri alisisitiza hapa kwamba Ziwa Victoria ni moja ya chanzo ambacho kitaendelea kutumika kwa sababu tayari tumeanza kukitumia kwa maeneo ya Kyerwa na Kyerwa ni Jimbo ambalo nimekwenda mara tatu mimi mwenyewe na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo, kwa hiyo, ni jimbo ambalo nimelifanyia kazi sana. Lengo ni kuhakikisha kwamba kwenye hili swali lako la pili kwamba lini kuona kwamba maeneo yote yatafanyiwa kazi kupata maji safi? Ndio kazi inayoendelea na ni maagizo ya Mheshimiwa Makamu wa Rais ambaye nilikwenda naye pale Kyerwa lakini na sisi kama Wizara tunaendelea kuyafanyia kazi Jimbo la Kyerwa.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni wananchi kiasi gani wa Wilaya ya Kyerwa wamefikiwa na huduma ya maji safi na salama?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafsi na mimi niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuishukuru Serikali kwa kutuletea Mradi wa Maji kutoka Lake Victoria ni lini sasa Serikali italeta mabomba ili kazi ianze kwa kasi kutokana na shida ya maji tuliyonayo? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Sitta kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni lini mabomba yatafika? Mwezi wa saba tunatarajia mabomba yawe yamefika kutoka India na tayari kazi zimeshaanza, wakandarasi wa miji 28 tayari wapo kazini. Nikupongeze kwa ufuatiliaji na nilishakuahidi kwamba tutakwenda pamoja Urambo na kuhakikisha mabomba yanaanza kufanya kazi. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni wananchi kiasi gani wa Wilaya ya Kyerwa wamefikiwa na huduma ya maji safi na salama?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Wizara tayari imeanza kutumia Mto Kagera kuwapatia wananchi wa Kyerwa maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali, Mradi wa Maji wa Kata ya Kimuli ambao unapeleka kwenye vijiji vitatu tayari umeanza, lakini mkanadarasi haendi vizuri kwa sababu bado hajalipwa pesa ya certificate ya kwanza; je, ni lini Serikali itamlipa mkandarasi huyu ili wananchi wa Kata ya Kimuli waanze kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee pongezi kwa sababu kazi inayofanyika ni kwa sababu ya ufuatiliaji wake makini, na kuhusiana na malipo ya mkadarasi Mheshimiwa Mbunge, sisi kama Wizara tunaendelea na michakato ya kuona wakandarasi wote tunakwenda kuwalipa kwa sababu ni wengi wako kwenye maandalizi ya malipo.