Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza vifo vya watoto wenye umri kati ya sifuri hadi mwaka mmoja?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu haya ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya asilimia 70 ya vifo vya watoto vya chini ya miaka mitano, vinatokea kati ya umri wa miaka sifuri hadi mwaka mmojal; je, Serikali haioni haja sasa kuweka mikakati mahsusi na kuwekeza kwa watoto wa umri huo mwaka sifuri hadi mmoja ili kupunguza vifo hivi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, katika Mkoa wangu wa Arusha moja ya sababu ambayo inapelekea vifo vya watoto wa chini ya mwaka mmoja ni ukosefu wa mashine za kuhifadhi watoto njiti; je, ni lini Serikali itapeleka vifaa hivi katika Hospitali zote za Mkoa wa Arusha? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge hasa kwa jinsi ambavyo anafanya ziara zake kwenye maeneo magumu hasa kwenye maeneo ya Mkoa wa Arusha yasiyofikika. Ni kweli anajua haya matatizo yapo, lakini umeona tulikotoka na mimi nimtoe tu Mheshimiwa Mbunge wasiwasi kwa sababu Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa sana katika eneo hili, kwa maana ya kuweka vifaa na mambo mengine na mmeona tulikotoka mambo makubwa kama CT Scan tulikuwanazo tatu nchi nzima lakini leo tuna zaidi ya 50, MRA mbili lakini leo tuna zaidi ya 19 kwa maana hili nalo ni dogo.

Mheshimiwa Spika, anachokisema Mheshimiwa Mbunge hapa ni kuongeza hiyo huduma. Kwa mwaka huu sasa tunaenda kujenga mia moja maana yake kwa swali lake la kwanza kwamba hilo la maeneo kufikika, maana yake zinajengwa mia moja, maeneo ya Mkoa wa Arusha ni maeneo ambayo pia hivi vituo 100 vinaenda kujengwa kwenye maeneo ambayo hayana.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni suala la kuweka vifaa vya kusaidia hao watoto ambao wanazaliwa kwa uzito mdogo. Ukijenga vituo mia moja na equipments zake zinawekwa kule ndani kwa hiyo hilo tatizo litakwenda kutoka na hakutakuwa na tatizo hilo tena.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza vifo vya watoto wenye umri kati ya sifuri hadi mwaka mmoja?

Supplementary Question 2

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, licha ya vifo vya watoto wachanga vilevile kuna tatizo kubwa la wazee kwa sababu hawana uwezo wa kulipa gharama na hata vile vitambulisho vinavyotolewa na Halmashauri wengi wa wazee huwa wanapata usumbufu.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa bima za afya kwa ajili ya wazee ili waendelee kupata huduma nzuri?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, suala hili la wazee kuwa na vitambulisho lakini hawapati huduma limekuwa likitokana na upungufu wa dawa na vifaa tiba ambapo hata Mbunge ni shahidi kwa sasa masuala ya upatikanaji wa dawa kwenye vituo vyetu umeongezeka. Kwa hiyo, hili sasa limeshatatuliwa kwa asilimia 78 kwenye vituo vyetu na hospitali zetu. Hivyo tutaendelea kuongeza mpaka zifike asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, pili, suala ambalo linaweza likatusaidia sisi kuondokana na hili tatizo moja kwa moja, ni sisi Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwamba ni lazima twende kwenye suala la Muswada wa Bima kwa Wote na ndilo suluhisho la kudumu kwa hilo. Lakini wakati huo kabla hatujafikia kwenye suala la Bima ya Afya kwa Wote kuna utaratibu wa kwamba mtu/mzee anayeshindwa kulipa kabisa na anayepata shida tunaweza tukatumia kwa maana ya kupata barua na mambo mengine, lakini sheria zetu vilevile zinatoa room kwa watendaji wetu kuwaaandikia barua na kupata huduma.