Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, kuna maamuzi mengine baada ya Kamati ya Mawaziri nane kurudisha kwa wananchi wa Itigi shamba la Kampuni ya Tanganyika Packers?

Supplementary Question 1

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kuna swali nauliza.

Mheshimiwa Spika, wale Mawaziri nane walikuja kufanya nini? Leo tunapokuja kusema kwamba Serikali haikuelekeza, haya kama huo ni mgogoro, je tutautatua lini? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; jambo la kwanza kwenye ile Kamati ya Mawaziri nane ambayo ilizunguka maeneo mbalimbali nchini, kila eneo lilikuwa linapelekewa taarifa kuhusiana na mahitaji ya eneo husika, sasa katika shamba la Kitaraka Holding maamuzi ya Serikali ambayo Kamati ya Mawaziri nane iliyatoa pale ni kwamba sasa ifanyike tathmini ambapo katika ile tathmini tutajua lile shamba wananchi wameingilia kwa kiwango gani ili sasa tuweze kumega sehemu ya lile eneo kuwakabidhi wananchi na sehemu ya eneo ibaki katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa ajili ya kazi ambayo ilikuwa inaifanya hapo awali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sasa hivi kinachofanyika, Kamati ya Mawaziri tulikaa na Mheshimiwa Waziri ikaundwa tume maalum ambayo inafanya hiyo tathmini na baada ya hiyo tathmini kukamilika sisi tutakwenda katika eneo hilo kwenda kutoa maamuzi ya mwisho kwa ajili ya wananchi. Kwa hiyo, hiyo ndio kazi kubwa ambayo imefanyika.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, kuna maamuzi mengine baada ya Kamati ya Mawaziri nane kurudisha kwa wananchi wa Itigi shamba la Kampuni ya Tanganyika Packers?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza.

Wananchi wa Mtaa wa Bangulo kwenye Kata ya Pugu Station walikuwa na mgogoro na shamba la Kabimita ambao Serikali iliumaliza kupitia Mawaziri wa Ardhi na Mifugo mwaka 2018 lakini mpaka leo wananchi wamefanya urasimishaji na Kabimita kupitia Wizara ya Mifugo haijakabidhi hati ya eneo hilo.

Je, ni lini sasa Serikali itaenda kukabidhi hati hiyo kwa Kamishina wa Ardhi ili wananchi wa Mtaa wa Bungulo Kata ya Pugu Station waweze kukabidhiwa hati yao na kuishi kwa amani?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Ukonga ka,a ifuatavyo:-

Ni kweli kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya kutatua migogoro tayari jambo hili tulikwishafika mwisho na Mheshimiwa Jerry kama ambavyo nimemjibu Mheshimiwa Massare katika swali la awali ni kwamba utaratibu wote ulikwisha kufanyika, wananchi wote ambao wanapaswa kupewa haki wanafahamika nani hatua tu za Kiserikali.

Sasa nitamwelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Kamishina wa Ardhi, jambo hili lifike mwisho na hatimaye hati iweze kuwa surrendered na wale ambao wanapaswa kunufaika, wanufaike na kama kuna malipo ya premiums ambazo wanatakiwa kufanya, wanatakiwa wafanye sawa na Sheria za Ardhi zinavyoelekeza, ahsante sana.