Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio sheria ya Manunuzi ya umma kwa kuwa ni kikwazo kwa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nishukuru Wizara kwa majibu mazuri yanayotia matumaini. Jambo hili linaenda kutatua tatizo kubwa la ununuzi, na hasa katika taasisi zetu za umma ambazo zinaingia kwenye ushindani ambazo zinashindwa kufanya manunuzi kwa sababu ya ushindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa miradi mingi kwenye halmsahuri zetu sasa hivi inatekelezwa kwa force account na watu wanaoingia kwenye manunuzi ni watu ambao hawana taalum; Je, Serikali iko tayari kutoa mwongozo mahsusi ili kuongoza kuona namna gani hayo manunuzi yanayokwenda kufanya kusiwe na mgongano ambao sasa hivi nani ambaye anatakiwa kujibu maswali hayo ya ununuzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ili kupunguza safari nyingi za maafisa ununuzi kwenda na kurudi kwa ajili ya kwenda kufanya manunuzi, Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza yale masurufi (imprest) kutoka milioni tatu ili kufika milioni kumi, kwa sababu sasa hivi hakuna bidhaa inayoweza kununuliwa kwa shilingi milioni tatu? Kwa hiyo matokeo yake wale maafisa manunuzi wanakwenda na kurudi zaidi ya mara tatu kwa bidhaa moja.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa ridhaa yako nijibu maswali yote mawili kwa pamoja. Taratibu, mwongozo na kanuni zinatolewa mara baada ya kutunga Sheria hiyo katika Bunge lako Tukufu. Hii ndiyo nafasi adhimu baada ya Muswada kuja Bungeni ya Wabunge kutushauri na kutuelekeza. Serikali yao ni sikivu sana tutaendelea kupokea ushauri huo na kuufanyia kazi, ahsante.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio sheria ya Manunuzi ya umma kwa kuwa ni kikwazo kwa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nami kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Manunuzi ya Umma inaelekeza asilimia 30 kwenda kwenye makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu lakini Sheria hii inaonekana kuto tekelezeka.

Je, ni lini Serikali itatilia mkazo Sheria hii ili iweze kuleta tija kwa jamii?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Njau kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii ipo na inatekelezwa. Tuna toa maelekezo kwa maafisa masuhuli wote ambao hawajatekeleza hili watuletee ripoti na tuwaambie kabisa watekeleze sheria hii kama ilivyowekwa.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio sheria ya Manunuzi ya umma kwa kuwa ni kikwazo kwa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Katika manunuzi ya Serikali kumekuwepo na utamaduni wa kuongeza bei bidhaa zinazonunuliwa na Serikali ukilinganisha na bei halisi iliyoko sokoni.

Je, Sheria hii mpya inayofanyiwa marekebisho itagusa eneo hili kuhakikisha Serikali inanunua kulingana na bei ya soko?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge katika hili. Itakapopita Sheria hiyo basi zitafuatwa taratibu zote za manunuzi katika bei halisi ambayo ipo nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufanya mapitio sheria ya Manunuzi ya umma kwa kuwa ni kikwazo kwa utekelezaji wa miradi katika Halmashauri?

Supplementary Question 4

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa miradi mingi ya Halmashauri inasimamiwa na walimu wakuu, waganga pamoja na walimu wakuu shule za msingi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa semina hao walimu wakuu baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa upya?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mpakate kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema awali taratibu, kanuni na miongozo itatoka mara tu baada ya Bunge lako Tukufu kupitisha Sheria hii. Naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subra itakapopita Sheria hii basi hayo yote anayoyatarajia yatapatikana.