Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita wanapata mkopo wa elimu ya juu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na hayo majibu yanayoridhisha kiasi, nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hawa wanafunzi wanaokwenda kusoma katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, naomba Mheshimiwa Waziri atuhakikishie kwa sababu hawa wa maendeleo ya jamii wanaegemea kwenye upande wa afya na elimu; je, wako katika kundi la kupata mikopo au ni wale wa VETA na vyuo vingine vya afya tu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya swali la msingi, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba inatoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu pamoja na wale wa elimu ya kati. Lakini naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatarajia kuanza kutoa mikopo kwa wanafunzi hawa wa elimu ya kati kama ilivyosomwa katika bajeti ya Serikali ya mwaka ujao wa 2023/2024 Serikali inatarajia kuanza kutoa mikopo kwa wananfunzi wa elimu ya kati katika kada za ualimu, afya pamoja na sayansi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kupanua wigo wa kutoa mikopo hii katika kada nyingine kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na uwepo wa bajeti, nakushukuru.

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanafunzi wote waliomaliza kidato cha sita wanapata mkopo wa elimu ya juu?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa fursa.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wanafunzi wenye ulemavu ambao wanafanikiwa kufika hatua hii ya elimu ya juu ni ndogo sana yaani idadi ya wanafunzi ambao wanafanikiwa kufika hatua hii ya eleimu ya juu ni ndogo sana, na kwa kuwa kundi hili linakabiliwa na changamoto nyingi za kimaisha.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa mikopo hii ya elimu ya juu kama ruzuku kwa kundi hili? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba miongoni mwa vigezo au sifa za upataji wa mikopo, mojawapo ni kwa wenzetu wenye mahitaji maalum wakiwepo watu wenye ulemavu. Kwa hiyo, kwanza tumeanza na kipaumbele kwa hawa, lakini tunatoa kama mikopo.

Mheshimiwa Spika, swali la Mheshimiwa Mbunge yeye anataka tufanye kama ruzuku, naomba tulichukue pendekezo lake hili au ushauri wake huu twende tukaufanyie kazi, tufanye tathmini ya wangapi hawa watu wenye ulemavu, na tuweze kuangalia namna bora ya kufanya, kama tulivyofanya kwenye Samia Scholarship, Mheshimiwa Rais alitoa fedha hizi zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya watoto waliofanya vizuri. Nadhani na hili la watoto wenye ulemavu linawezekana, nakushukuru.