Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya kuigawa Shule ya Msingi Mwanhuzi kwa kuwa shule hiyo ina wanafunzi 1,400?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na kazi nzuri iliyofanywa na Serikali naomba kuuliza swali moja tu la nyongeza.

Shule husika ililetewa fedha shilingi milioni 80 kwa ajili ya kujenga bweni la watoto wenye mahitaji maalum, je, ni lini Serikali italeta fedha za kukamilisha bweni hilo? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Komanya amekuwa akifuatilia sana shule hii ya Mwanhuzi na alinieleza nilipokutana naye ofisini kwamba ndipo alipotokea yeye kwenye kata hiyo na atahakikisha kwamba fedha hii shilingi milioni 348 inapatikana, kwa hiyo, nimpongeze sana Mheshimiwa Leah kwa hili.

Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la nyongeza la bweni ambalo lilianzwa kujengwa katika shule hii hii ya Msingi ya Mwanhuzi. Serikali ilipeleka shilingi milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa bweni kwa watoto wenye mahitaji maalum katika shule hii na sio shule hii pekee yake bali ilipeleka nchi nzima kwa ajili ya ujenzi wa mabweni haya, lakini baada ya kupeleka fedha hizi ujenzi ule haukukamilika na changamoto hii tunaifahamu na timu ya wataalam ilitumwa kwa ajili ya kufanya tathmini kwenye mabweni yote na mabwalo yote ambayo yalipelekewa fedha na hayakukamilika. Baada ya tathmini hiyo kufanyika sasa tupo katika mchakato wa kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka kukamilisha ujenzi wa mabweni haya na mabwalo haya. (Makofi)