Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini katika Mkoa wetu wa Katavi katika Jimbo la Nsimbo tuna x-ray ambayo Serikali imetupatia lakini x-ray hiyo imeshindwa kufanyakazi kutokana na kwamba hatuna mtaalam wa mionzi.

Je, ni lini Serikali itatupatia mtaalam wa mionzo ili x-ray iweze kufanyakazi kwa kuwahudumia wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili; katika Wilaya ya Tanganyika Kata ya Ilangu wananchi ususani kinamama wajawazito wamekuwa wakifata huduma mbali sana kutokana na kwamba hawana kituo cha afya; je, ni lini Serikali itatujengea kituo cha afya katika Kata hiyo ya Ilangu? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Martha Mariki, la kwanza hili la wataalamu wa mionzi, hivi karibuni katika mwaka huu wa fedha Serikali imeajiri watumishi wa kada ya afya 8,000 na tayari katika matangazo yale wakati yanatolewa ilikuwa tunatafuta watalamu wa mionzi ya x-ray 69. Lakini nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba katika ajira hizi walipatikana watumishi 61 tu na hizi nafasi nyingine zilizosalia tutazitangaza upya ili kuweza kuwapata watalam hawa wa mionzi na tuweze kuwapeleka maeneo mbalimbali nchini ambapo Serikali imewekeza fedha nyingi katika ununuzi wa vifaa tiba ikiwemo mitambo ya mionzi na kule Nsimbo napo tutapaangalia kwa ajili ya kuwapeleka watalamu hawa wa mionzi.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la Kituo cha Afya katika Kata ya Ilangu iliyopo kule katika Wilaya ya Tanganyika, tutatuma timu ya watalaam kwa ajili ya kwenda kufanya tathimini katika Kata ya Ilangu, kuona idadi ya watu waliokuwepo pale na vile vigezo vinavyotakiwa vya umbali kwenda kufata huduma ya afya na kadhalika na baada ya tathimini hiyo kufanyika tutapata taarifa katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kuweka katika mipango yetu kuhakikisha kwamba wananchi wa Kata ya Ilangu wanapata huduma ya afya iliyobora kwa kupata kituo cha afya.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Kwa kuwa kituo cha afya cha Kata ya Nyang’hwale kinatoa huduma zaidi ya miaka 30 kuhudumia kata zifuatazo; Kata za Shabaka, Kaboha, Busolwa, Nyabulanda, Nyijundu, Mwingiro hakina huduma ya x-ray je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka huduma hiyo ya x-ray kwenye Kituo cha Afya cha Nyang’hwale? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia imeweka kipaumbele katika kuhakikisha wananchi wake wanapata afya iliyobora kwa kuwekeza kwenye miundombinu ya afya vilevile kwenye vifaa tiba na katika bajeti ya mwaka 2023/2024 Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba ikiwemo vifaa vya mionzi kama vile x-ray na pale tutapoanza ununuzi wa vifaa hivi tiba tutaweka kipaumbele kwa ajili Kituo cha Afya cha Kata ya Nyang’hwale anapotoka Mheshimiwa Amar kule. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupeleka vifaa tiba vya kisasa katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang kama ventilator, anesthesia machine na diathermy ili koboresha huduma za afya ya mama na mtoto? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba hospitali zote za Wilaya zinakuwa zina vifaa tiba vya kisasa na tayari tumeshapeleka fedha kwa wenzetu wa MSD kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba. MSD imeanza kupeleka vifaa hivi katika Hospitali za Wilaya mbalimbali hapa nchini. Nitakaa na Mheshimiwa Hhayuma kuweza kuona Hospitali ya Wilaya ya Hanang ipo katika awamu ipi ya kupokea vifaa tiba hivi vya kisasa katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Supplementary Question 4

MHE ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha Afya cha Ngw’angw’ali na Ngulyati Wilaya ya Bariadi kina upungufu wa vifaa tiba; je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba vya kutosha? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kuhusu upelekaji wa vifaa tiba Bariadi kama nilivyotoka kusema hapa awali, Serikali katika mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga kiasi cha shilingi bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kote nchini na katika hivyo tutahakikisha yale maeneo yenye uhitaji mkubwa yanapata vifaa tiba hivi ikiwemo kule Bariadi alikokutaja Mheshimiwa Midimu.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya vifaa tiba katika Hospitali za Wilaya zinazojengwa?

Supplementary Question 5

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia watu wengi sana pale, nini mkakati wa Serikali kuongeza vifaa tiba vya kisasa? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali hii ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha kwamba vifaa tiba vya kisasa vinakuwepo katika hospitali zote za Wilaya na vilevile katika vituo vyetu vya afya vya kimkakati. Katika kuhakikisha hilo linafanyika Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba hivyo vya kisasa na tutahakikisha pia Hospitali ya Mji wa Mafinga nayo inaongezewa vifaa tiba kama ilivyofanyiwa katika mwaka wa fedha huu tunaomaliza sasa.