Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti ili kubaini mazao yanayoweza kulimwa na kustawi Mkoa wa Mtwara kama mbadala wa zao la korosho?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza nataka kujua mkakati wa Serikali wa kuhakikisha unawapatia mbegu bora kwa ruzuku wakulima wa mazao haya mengine.

Swali langu la pili, nataka kujua kuna changamoto kubwa sana ya masoko hasa ya zao la muhogo pamoja na mbaazi wakulima wanalima lakini wanakosa masoko ya uhakika. Nataka kujua mkakati wa Serikali kuhakikisha masoko ya mazao haya yanapatikana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upatikanaji wa mbegu kwa ajili ya wakulima kwa mfumo wa ruzuku. Sisi kama Serikali tuko tayari kuhakikisha kwamba tunaongeza uzalishaji wa mazao haya na pindi pale mahitaji yakiainishwa kupitia TARI na ASA tupo tayari kuwapatia wakulima mbegu hizi katika mfumo wa ruzuku ili waweze kuongeza uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu masoko ya uhakika, nikianza na mbaazi, kwenye mbaazi tayari tumeshaingia makubaliano ambayo bado tuko katika hatua za mwisho na Serikali ya India ya kuchukua zaidi ya tani 150,000 na hivi sasa ninavyozungumza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo yuko India kwa ajili ya kufatilia jambo hili hili kuhakikisha kwamba tunapata soko la uhakikia la wakulima wa mbaazi ili kuondokana na changamoto hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hili pia kupitia TARI na MDT ambayo ni taasisi inayo jishughulisha na masuala ya masoko ya mazao, tumeendelea kutoa elimu na mafunzo juu ya matumizi ya ziada ya mbaazi ikiwemo lishe lakini pamoja na matumizi mengine ya viwanda kwa ajili ya kuongeza soko la zao hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Muhogo tunao mkakati wa kitaifa wa kuendeleza zao la muhogo wa mwaka 2020 mpaka 2030 ambao ndani yake pia umeainisha mikakati mbalimbali ikiwemo kuwahusisha watu wenye viwanda kwa ajili kutengeneza wanga kupitia muhogo, industrial of starch wanaita ili tuongeze soko la muhogo wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tupo katika mawasiliano na ubalozi wa China, Rwanda na Burundi kuongeza wigo mpana wa soko la muhogo ili kuwaondolea changamoto wakulima juu ya upatikanaji wa uhakika wa soko la muhogo.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti ili kubaini mazao yanayoweza kulimwa na kustawi Mkoa wa Mtwara kama mbadala wa zao la korosho?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Je, Serikali imejipangaje kushajihisha, kuongeza uzalishaji wa mazao ya nafaka asilia kama fiwi, mtama, uwele, ufuta, dengu,choroko na mbaazi kwa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya kilimo hiki?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejipanga kuanzisha kanda za kilimo Tanzania Agricultural Growth Corridor ambalo lengo lake kubwa ni kulima mazao kutokana na afya ya udongo itakavyoruhusu. Kwa hiyo, tunaendelea na kazi ya upimaji wa afya ya udongo, yale maeneo ambayo mazao uliyosema yanastawi tutayapa kipaumbele na tutatenga maeneo ili wakulima wapate maeneo ya kutosha na waweze kunufaika zaidi kupitia mazao hayo.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti ili kubaini mazao yanayoweza kulimwa na kustawi Mkoa wa Mtwara kama mbadala wa zao la korosho?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuendelea kugawa miche bora ya kahawa yenye ukinzani dhidi ya magonjwa sugu ya kahawa kwa wakulima wa Jimbo la Moshi Vijijini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Mibuni tuliyonayo asilimia kubwa imeshakaa zaidi ya miaka 25 na hivyo kupunguza uzalishaji, hivi sasa Serikali kupitia TAKRI na wadau wengine kama bodi ya kahawa tutahakisha kwamba tunazalisha miche ya kutosha na hasa kupitia teknolojia ya chupa ili wakulima wengi zaidi wapate miche iwafikie kwa urahisi na waweze kuongeza uzalishaji ikiwemo wa kulima wa jimboni kwa Mheshimiwa Prof. Ndakidemi.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti ili kubaini mazao yanayoweza kulimwa na kustawi Mkoa wa Mtwara kama mbadala wa zao la korosho?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Zao la pamba ni miongoni mwa mazao yanayofanya vizuri katika Mkoa wa Mtwara lakini zao hili limezuiliwa kulimwa Mkoa wa Mtwara kutokana na ugonjwa ambao upo kwenye zao la Pamba Nchini Msumbuji Jimbo la Kabodayogado. Je, ni lini Serikali itaondoa zuio hili?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunalo tishio la funza wekundu ambao wanapatikana katika nchi za Msumbiji pamoja na Zambia na maeneo mengineyo. Kwa sababu ya tishio hilo tumeendelea kuweka quarantine na tuna sisitiza tu wananchi wa Mkoa wa Mtwara kuendelea kulima mazao mbadala kama ufuta, korosho lakini kwa hivi sasa kwenye pamba tunayo changamoto kubwa na hatuwezi kuachia hivi sasa kwa sababu ya tishio la hao funza wekundu.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya utafiti ili kubaini mazao yanayoweza kulimwa na kustawi Mkoa wa Mtwara kama mbadala wa zao la korosho?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na ucheleweshaji wa mbegu kwa wakulima na hivyo wakulima kukosa tija kwenye kilimo chao. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha mbegu zinapelekwa kwa wakati ili waweze kulima kwa tija? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, changamoto kubwa ya upatikanji wa mbegu kwa wakati ilikuwa ni kwamba mzalishaji mkubwa wa mbegu ASA alikuwa na yeye alikuwa anategemea mvua kama ambavyo mkulima kuzalisha mbegu. Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mama Samia Suluhu Hassan tumetenga fedha kuhakikisha kwamba tunaanza kuweka miundombinu ya umwagiliaji katika mashamba yetu ya mbegu ili tuwe tuna uwezo wa kuzalisha mbegu mwaka mzima na wakulima wazipate kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanzia katika mashamba yetu makubwa nane ya awali tumeweka miundombinu center na lateral pivot kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunamwagilia mashamba haya na mbegu zinapatikana kwa mwaka mzima na zitawafikia wakulima kwa wakati na msimu ukianza watakuwa nazo.