Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kusaidia Halmashauri zinazozunguka Mbuga/Hifadhi za Taifa kupitia CSR kutoka kwenye mapato ya utalii?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Wizara na taasisi zake zinatekeleza miradi hiyo moja kwa moja badala ya kupitia halmashauri.

Je, hawaoni sasa ni muda muafaka fedha hizo zitengwe zipelekwe halmashauri ili halmashauri itekeleze kwa usawia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwenye Mkoa wa Kilimanjaro tumepitisha sheria kali sana za mazingira zinazozuia kukata miti kwa ajili ya kutunza mandhari ile na hali ya Mlima Kilimanjaro, jambo linaloleta usumbufu kupatikana kwa nishati ya kupikia kwa wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Je, hatuoni sasa kwa Mkoa wa Kilimanjaro ni muda muafaka fedha hiyo ya CSR tuitumie kuwaletea wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro nishati mbadala ya bei nafuu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ya fedha hizi ni kuhakikisha kwamba zinakwenda moja kwa moja kwenye community, kwa maana ya kwamba kwenye jamii. Hatuna shida na halmashauri lakini tumeona fedha hizi bora ziende moja kwa moja kutoka kwenye taasisi husika kwenda kwenye jamiii moja kwa moja kwa sababu kwanza tumeona jamii iweze kujua mchango wa uhifadhi na vipi wanaweza kunufaika na maeneo yale yaliyohifadhiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili tumeona kwamba, miradi mingi imekuwa inasuasua, sasa tukaona tukizipeleka fedha moja kwa moja, miradi hii itapata kumalizika kwa haraka na jamii iweze kunufaika. Kikubwa zaidi tumeona miradi ambayo inahitajika ndiyo iende kwa jamii. Kwa hiyo kikubwa nimwambie Mheshimiwa kwamba wazo lake sawa tunaweza kulichukua tukaona namna ya kulifanyia kazi, lakini kwa sasa tumeona bora fedha moja kwa moja ziende kwa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nimwambie kwamba, fedha hizi ziko kwa ajili ya miradi mbalimbali ikiwemo maji, umeme, zahanati na hata shule, lakini vile vile tu kwa kuwa sasa suala la nishati mbadala kwa sasa ni ajenda ya kitaifa, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili alilolishauri tunalichukua, tunakwenda kulifanyia kazi ili tuone namna ambavyo tunaweza tukachota fedha kutoka kwenye fungu hili na kuweza kushughulika na masuala ya nishati mbadala kwa sababu ndio ajenda ya Kitaifa, nakushukuru.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kusaidia Halmashauri zinazozunguka Mbuga/Hifadhi za Taifa kupitia CSR kutoka kwenye mapato ya utalii?

Supplementary Question 2

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniruhusu kuuliza swali la nyongeza. Hifadhi za Taifa na Mapori ya Akiba imekuwa ni moja ya chanzo cha migogoro mikubwa kati ya wananchi na taasisi za Serikali, lakini kutokushirikisha wananchi kupitia sera hiyo ya uwajibikaji kwa jamii imekuwa ni moja ya vyanzo vya migogoro hii. Je, Serikali inaweza ikatoa tamko ni kwa nini fedha za CSR hazijaenda kwa wananchi ambao wanapakana na Hifadhi ya Mikumi kwa miaka sita mfululizo? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali hilo la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la fedha hizi ambazo kama ambavyo tumeeleza zinazotoka kwenye taasisi zinazosimamia uhifadhi. Lengo na madhumuni moja kwa moja ziende kwa wananchi, lakini changamoto iliyokuwepo ni moja kwamba fedha hizi haziwezi kutosheleza kupeleka kwenye Halmashauri zote kwenye maeneo yote. Kwa hiyo nimwambie tu Mheshimiwa, moja ni kwamba tunawashirikisha na ndiyo maana tukamjibu Mheshimiwa pale kwamba fedha hizi ni bora ziende moja kwa moja kwa wananchi ili tuwashirikishe na tuweze kujua wanachokitaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutakapopata fedha, tutahakikisha kwamba kwenye Halmashauri yake na maeneo yake fedha hizi zinafika na zinatekeleza miradi ya wananchi.

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kusaidia Halmashauri zinazozunguka Mbuga/Hifadhi za Taifa kupitia CSR kutoka kwenye mapato ya utalii?

Supplementary Question 3

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya utekelezaji wa CSR kupitia Halmashauri. Kwa ushauri wangu, je, Wizara sasa haioni haja ya kuja na sheria na kanuni kabisa ambazo zitawa-guide watu wa hifadhi pamoja na wanaofanya shughuli za kiutalii zaidi ili lile suala la CSR liwe suala la kisheria kabisa? Nashukuru.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wake tunauchukua na tutakwenda kuufanyia kazi. Nashukuru.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kusaidia Halmashauri zinazozunguka Mbuga/Hifadhi za Taifa kupitia CSR kutoka kwenye mapato ya utalii?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za CSR katika Vijiji vinavyopakana na Pori la Akiba la Selous vya Zinga Kibaoni, Mtepela, Namatewa pamoja na Ngarambi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha katika Halmashauri hizo na maeneo aliyoyataja zitafika cha msingi Mheshimiwa Mbunge awe na subira, tutafute hizo fedha ili tuone namna ya kuja kusaidia wananchi katika maeneo hayo na wao waweze kunufaika na uhifadhi, nakushukuru.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani kusaidia Halmashauri zinazozunguka Mbuga/Hifadhi za Taifa kupitia CSR kutoka kwenye mapato ya utalii?

Supplementary Question 5

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa waboreshaji wakubwa wa mazingira ni wanawake wakiwemo wanawake wa Kilimanjaro wnaaouzunguka mlima; na kwa kuwa hawa watu wanaotoa CSR wankwenda zaidi kwenye miradi mikubwa wakiacha kugawa miche na kuhakikisha kuwa miche ile inatunzwa na kuweza kufikia katika hali ya kurudisha uoto wa asili. Je, ni lini sasa taasisi hizo ikiwemo TFS wataweza kushirikiana na wanawake wa Kilimanjaro ambao wana nia sana ya kuboresha mazingira hayo kutokana na jambo alilolifanya Mheshimiwa Rais la Royal Tour kugawa miche ya matunda na miche ya kuboresha mazingira na kurejesha? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna uharibifu mkubwa wa mazingira maeneo hayo hasa yanayozunguka Mlima wa Kilimanjaro. Uharibifu ambao unasababishwa na shughuli za kibinadamu na hapa tunataka tuchukue fursa hii tutoe maelekezo tuwaambie wananchi, tuwashauri sana, waache kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo haya zikiwemo za ufugaji na mambo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutajitahidi tupeleke fedha kwa Mkoa huu wa Kilimanjaro, hasa kwa akinamama, lengo na madhumuni ikiwa ni kuweza kurejesha ile hali katika ule Mlima Kilimanjaro. Nakushukuru.