Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mabwawa katika Mito Ghona, Rau na Deu ili kupunguza athari za mafuriko?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri na yenye tija, naomba niulize maswali mawili madogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Jimbo la Vunjo kuna mabwawa mawili moja linaitwa Urenga katika Kata Kirua Vunjo Mashariki na nyingine ni Koresa Kata ya Kirua Vunjo Kusini yameharibika sana sasa hivi ni kama vile hayapo. Nataka nijue kama Waziri atakubali kutembelea eneo hili na kuyaona haya mabwawa ili aone kama watafanya nini kuyakarabati? (Makofi)

Swali la pili. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu ukamilishaji wa miradi iliyoanza mwaka juzi kule Mamba Kaskazini na Kusini, Mwika Kaskazini na Kusini na Marangu Mashariki na Magharibi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Charles Kimei kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kutembelea mabwawa ambayo kwa sasa hayafanyi vizuri. Mheshimiwa Mbunge, naomba nikuhaidi baada ya Bunge hili tutakwenda kuyatembelea na kuona nini kinaweza kufanyika kupitia watalaam wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na kukamilisha miradi Mheshimiwa Mbunge pia hili tutakapokuwa tunatembelea tutaona kwa nini miradi hii haijamilika kwa wakati? Nakuhakikishia tutahakikisha inakamilika ili wananchi waweze kupata huduma. (Makofi)