Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 1

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa duniani kwa sasa, watu zaidi ya 28 wanakufa kila sekunde kwa sababu ya magonjwa yasiyoambukiza na kwa sababu Tanzania kwa sasa kisababishi kikubwa cha vifo Tanzania ni magonjwa yasiyoambukiza. Kwa nini Serikali isitoe fedha za kutosha ili wananchi waweze kupata elimu, wajue visababishi, wajue na namna ya kujikinga kwa sababu haya magonjwa yanaweza kuzuilika?

Mheshimiwa Naibu Spika, tumbaku ni zao la biashara ndani ya Tanzania, lakini tumbaku hiyo hiyo ni kisababishi kikubwa kinacholeta magonjwa yasiyoambukiza kama kansa, stroke, presha na kisukari. Je, ni lini Serikali itawawezesha wakulima wa tumbaku nchini ikawapa mazao mbadala, wakawatafutia na masoko ili kusudi waondokane na hiki kilimo ambacho kinaathiri afya zao? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuja na swali hili zuri ambalo ni eneo kwa kweli ambalo Mheshimiwa Waziri wa Afya ameliwekea msisitizo wa nguvu sana kwa sababu ndiyo tatizo kubwa kwa sasa kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza; kwanza Serikali imeweka fedha nyingi kwa sababu ukiona kwenye miundombinu, lakini ukiona manunuzi ya CT scan na mambo mengine, lakini Wabunge wamemwona Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan hapa karibuni alisaini mikataba na Wakuu wa Mikoa kwenye eneo hili la lishe. Pia wameona viongozi mbalimbali wakishiriki katika matamasha makubwa. Kwa hiyo fedha tulizotaja hapa ni fedha tu kwa ajili ya hamasa, lakini hatujazungumzia kwa ujumla dawa na sehemu zingine mtambuka ambazo fedha zimewekezwa kwa ajili ya eneo hilo. Kwa hiyo kuna fedha za kutosha na tutaendelea kuona ni namna gani tutasisitiza eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu tumbaku; kupanga ni kuchagua, ni ukweli kabisa kama ambavyo Mbunge anasema tumbaku ina madhara mengi, siyo tumbaku tu pekeyake pamoja na kelele zinazopigwa mitaani pamoja na mambo mengine mengi ambayo tunayatumia. Sasa Mheshimiwa Mbunge pamoja na ukweli huu wa kwamba tunahitaji kutafuta zao mbadala wa tumbaku, naomba nisiseme lolote hapa kwa sababu linahusu Wizara zote na taratibu zetu na maslahi ya wananchi, tutashirikiana na Wizara husika na tuone ni namna gani tunaweza kufanya, lakini kweli kuna tatizo hili na siyo tumbaku peke yake kuna mambo mengi yanayosababisha tatizo hilo. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali; je, mpango ukoje kwa Bima ya Afya kwa Wote kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa hawa wa magonjwa yasiyoambukiza?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa bima ya afya ulikuja hapa kwa ajili ya sisi kuja na Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ili kuweza kabisa kuboresha mambo mengi ambayo yangeweza kusaidia pamoja na eneo hili tunaloliona. Kwa hiyo kikubwa mimi na wewe tuendelee kushirikiana kuona ni namna gani tunapambana kupeleka Muswada wetu wa Bima ya Afya kwa Wote uweze kurudi na iwe ajenda ya Mbunge ya kudumu na ajenda ya kudumu ya Wabunge ili wananchi waweze kupata huduma tukija na mpango wa Bima ya Afya kwa Wote. (Makofi)

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza?

Supplementary Question 3

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na tabia wagonjwa wa magonjwa ya kuambukiza wakienda kwenye dispensary na vituo vya afya hawapewi dawa za magonjwa ya kuambukiza kama presha. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha inatoa dawa kwa wagonjwa wetu hata huku kwenye ngazi ya dispensary na vituo vya afya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachokisema Mheshimiwa Mbunge tulikuwa na tatizo hili, lakini kama Wabunge wanakumbuka juzi nilijibu swali kwamba kwenye eneo la dispensary zimeongezeka dawa zinazotolewa kutoka 243 mpaka 459, maana yake madawa hayo ya presha, sukari yameongezwa kwenye level ya dispensary, kwa hiyo tatizo hilo halitakuwepo tena. (Makofi)