Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni kwa nini Wananchi wanaotumia Bima ya Afya wanalalamika kuhusu huduma wanazopatiwa?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana na nashukuru pia majibu ya Serikali nimeyasikia. Lakini wananchi wapokata Bima ya Afya wanajua wameweka akiba kwa ajili ya matibabu pale wanapoumwa kumekuwa na utofauti wanapokwenda hospitalini kupata huduma wanaambiwa bima yako daraja lake huwezi kupata dawa hizi, huwezi kupata huduma hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuwapa elimu mapema kabla hawajakata bima ili kujua kwamba bima yake anaweza kupata matibabu gani kwenye eneo lipi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa NHIF na Serikali mmekili kwamba bado kuna changamoto na changamoto hizo na CAG naye amezungumza usimamizi mbovu pamoja na taarifa za uongo zinapotolewa. Ni upi mkakati wa Serikali wa kumaliza changamoto hizi ili kurudisha dhana ile kwa Serikali kuliko hivi sasa wananchi wanaamini hatuna maana tena ya kuwa na Bima ya Afya? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri lakini naomba tu nimwambie kwamba kwenye eneo la NHIF hakuna madaraja labda akiwa amechanganya kati ya NHIF na CHF. Kwenye CHF ndiyo kuna madaraja kwa maana kuna kutibiwa kwenye kunafikia level fulani hutibiwi level fulani na mambo mengine kama hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tulikuja na mkakati wakati wa kuja na Muswada wa Bima ya Afya kwa watu wote tulikuja na mkakati thabiti wa kuboresha eneo la CHF pamoja kwamba tunayo Bima ya Afya kwa wote. Lakini tuone kwa uwezo pili hicho kwa sababu hatufuti CHF lakini tukaja na makakati wa kuboresha ili kuondoa madaraja ambayo Mheshimiwa Mbunge anayazungumzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nataka kukuhakikishia kwamba matatizo watu wako wa Nkasi wanayoyapata kutokana na hayo mambo tukikubaliana pamoja kwamba baada ya muda tutakuja na Muswada wa Bima ya Afya kwa wote tutaweza kutoa hilo tatizo. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni kwa nini Wananchi wanaotumia Bima ya Afya wanalalamika kuhusu huduma wanazopatiwa?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua, hivi karibuni kumekuwa na utata sana wa Bima ya Afya CHF kwa wananchi wa vijijini. Hii bima imefutwa au ipo? Nini tamko la Serikali? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, bima hii haijafutwa na tunashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ambao ndiyo wanasimamia eneo hili la CHF ili kuona katika kipindi hiki cha mpito ambacho kuna haya matatizo ambayo Wabunge mnayazungumzia tunaboreshaje pamoja sisi na TAMISEMI tuone ni namna gani tunaiboresha ili kuondoa matatizo yayosemwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mojawapo kuna wenzetu ambao wanafadhili eneo hili kuna Taasisi inafadhili eneo hili wanasaidia kwenye matangazo wanasaidia kwenye kuhamasisha, tunataka tukae nao pamoja tuone namna gani badala ya kufanya matangazo, kufanya warsha na tamasha warudishe hizo fedha waende kuboresha kwenye eneo la kitita ili wananchi kuweza kuondokana na tatizo hili. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni kwa nini Wananchi wanaotumia Bima ya Afya wanalalamika kuhusu huduma wanazopatiwa?

Supplementary Question 3

MHE. ENG. EZRA J. CHILEWESA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Hospitali ya Wilaya Biharamulo tulianza kutoa huduma tarehe 13 Januari, tukapata usajili tarehe 20 Februari. Lakini mpaka sasa tangu tume-apply maombi kwa ajili ya kutoa Huduma za NHIF kwenye hospitali yetu hatujapata kibali wala hatujapata majibu kutoka NHIF. Ni nini kauli ya Serikali juu ya wakazi wa Biharamulo wanaotumia hospitali ile kwa sababu wamekosa haki yao ili hali wanazo kadi na wana kila kitu kinachohusu NHIF. Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimeanza kumjua Mheshimiwa Mbunge kwa yeye kupigania hii hospitali yake. Kwa hiyo, kwa kweli sisi kama Serikali hatutakubali kazi uliyofanya kwa nguvu kubwa kwa miaka miwili wananchi wasiweze kupata huduma. Kwa hiyo, namwagiza Mkurugenzi wa NHIF Taifa nampa siku tatu Hospitali yako ya Biharamulo ipate Mfuko wa NHIF.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, ni kwa nini Wananchi wanaotumia Bima ya Afya wanalalamika kuhusu huduma wanazopatiwa?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana niliuliza kwamba kwa kuwa na nyinyi Serikali mmekiri kwamba kuna changamoto kwenye aina ya Bima hiyo ya CHF kwamba mkakati wa Serikali ni upi wakumaliza changamoto hizo ili kuondoa hii dhana ambayo wananchi wanayo sasa kuona hakuna haja ya kuwa na Bima ya Afya wanapoenda kwenye huduma. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachosema Mheshimiwa Aida nimekwenda pamoja na yeye kwenye jimbo lake nimeona hilo tatizo na wananchi wamekuwa lalamika. Kwanza nikupongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi ulivyo karibu na nilivyopita kule nilikuwa nashangaa ulishindaje kule kwa ile structure? Nikajua hapo sasa hivi kwa kweli wewe ni mwanamke wa shoka kwa ushindi uliyopata pale Nkasi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tu kwamba, tumesema hapa moja nimeeleza kwa swali alilosema mwenzetu Mbunge pale kwamba kwakweli kwa sasa tunashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ambao wanasimamia eneo hilo kwamba tuone kwa kipindi hiki cha mpito ambao bado Muswada wa Bima ya Afya kwa wote haujaja tunakaaje tuweze kuboresha eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ni kwa sababu kuna taasisi ambayo ina support eneo hili na Waziri wa Afya ameishawaita tuone tunakaaje waweze kukaa. Fedha wanazotumia kwenye warsha, matangazo na nini wanaweza kuboresha hicho kitita wakati tunangojea Muswada wa Bima ya Afya kwa wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mimi mwenyewe eneo hilo la CHF sithubutu kulipigania kule jimboni kwangu. Kwa sababu ukipigania halitoi matokeo unayotegemea lakini naamini kwa ushirikiano wetu na TAMISEMI tumeweka mkakati mzuri sana ambao tutaboresha eneo hilo baada ya muda siyo mrefu.