Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa fedha hizi tayari zimeshatengwa:-

(a) Je, ujenzi huu utaanza mwezi gani?

(b) Je, uko tayari tufuatane kwa pamoja ili kwenda kujiridhisha hali halisi ilivyo kwa nyumba zile? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, fedha hizi zimetengwa katika Bajeti ijayo 2023/2024. Kwa hiyo, wakati wowote baada ya mwezi Julai fedha zitakapotoka na ujenzi ukaanza, niko tayari kuongozana na Mbunge ili kwenda kushuhudia maendeleo ya ujenzi huo, nashukuru. (Makofi)

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia ukarabati nyumba za Polisi zilizopo Madungu Wilaya ya Chake Chake?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitembelea eneo la Chake Chake na kubaini mbali ya uchakavu wa Kituo cha Polisi cha ngazi ya Wilaya, vile vile nyumba za Askari zimechakaa sana. Hata hivyo, Serikali imeanza kujenga hanga moja ambalo litachukua Askari lakini tutaendelea kuzikarabati nyumba hizo kadiri tunavyopata fedha ili Askari wote waweze kukaa kwenye makazi yenye hadhi stahiki, nashukuru. (Makofi)

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, ni lini ujenzi wa nyumba ya Kamishna wa Zanzibar itajengwa kwa vile hivi sasa anakaa uraiani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kutokuwepo kwa nyumba yenye hadhi anakaa Kamishna wa Polisi ZanzIbar na katika bajeti hii inayoendelea tumeweza karabati ofisi ya kamishna. Hatua itakayofuata katika bajeti ijayo ni kuhakikisha kwamba nyumba ya Kamishna wa Polisi Zanzibar inajengwa na kukamilishwa, ahsante.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 4

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante napenda kuuliza swali. Nyumba za askari polisi Wilayani Maswa ni za siku nyingi sana zimejengwa na mkoloni je, ni lini Serikali itajenga nyumba hizo upya ili ziwe na hadhi ya kuishi askari polisi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwa upande wa Maswa si nyumba tu ambazo zimejengwa wakati wa mkoloni. Hata kituo cha polisi ngazi ya wilaya hakipo chenye hadhi stahiki. Katika bajeti ijayo tutaanza utaratibu wa kuweka fedha kwa ajili ya ujenzi wa hizo nyumba, lakini na kuanza kujenga kituo cha polisi chenye hadhi wilaya kama ambavyo imewahi kuulizwa na Mbunge wa Jimbo husika na tukamjibu hapa, ahsante sana.

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 5

MHE. OMAR ISSA. KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante je, ni lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Jeshi la Polisi Wilaya ya Micheweni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kadri ambavyo tutapata fedha tutaendelea kuimarisha na kujenga Vituo vya Polisi na Makazi ya Askari. Kwa hiyo, Micheweni ni moja ya eneo litakalozingatiwa katika ujenzi wa nyumba za askari, ahsante. (Makofi)

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 6

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuwa Kituo cha Polisi Chimala ni duni na makazi ya askari wale ni duni je, lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo hicho pamoja na makazi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua jinsi ambavyo Chimala kunaendelea kwa kasi kule Mbarali na niwapongeze wananchi wa Chimala pamoja na uongozi wao akiwemo Mbunge na DC kuanza Ujenzi wa Kituo cha Polisi Chimala na hatua itayofuata ni kuingia ujenzi wa nyumba za makazi ya askari. Serikali itawaunga mkono pamoja na wadau kama ambavyo RPC ameanza kufanya ili kuhakikisha kwamba Chimala wanapata nyumba bora za kuishi, ahsante. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza:- Je, lini Serikali itawajengea nyumba za kuishi Askari wa Jeshi la Polisi waliopo Kengeja?

Supplementary Question 7

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali langu kule Makete hamna Nyumba za Jeshi la Polisi, ukienda Dodoma hapa nyumba za askari polisi hapa hazifai, ukienda Oster Bay Dar es Salaam hazifai ni upi mkakati mahususi wa Serikali wa kujenga nyumba za polisi nchini kama ambavyo JWTZ imefanya kwa ajili ya maaskari wao? Kwa hiyo tunaomba majibu ya Serikali kwa kushirikiana na National Housing.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa swali la mkakati zaidi. Niliwahi kueleza hapa katika moja ya maswali kwamba Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi inao mpango wa miaka kumi wa ujenzi na ukarabati wa Vituo vya Polisi na Makazi kwa ajili ya Askari. Kwa hiyo, mpango tunao kazi tuliyonayo ni kutafuta fedha kadri tunavyoendelea utekelezaji tunapata fedha kutoka kwenye tozo lakini tutapata fedha kutoka kwenye bajeti ya maendeleo kwa madhumuni ya kujenga vituo na nyumba hizo. Kwa hiyo, maeneo yote yatafikiwa kadri ya upatikanaji wa fedha. (Makofi)