Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Ikana – Chitete pamoja na kujenga kwa kiwango cha lami barabara za milimani?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nilitaka tu kusema kwamba, pamoja na kuchimba miamba hiyo, barabara hiyo bado magari hayawezi kupanda. Kwa hiyo, pamoja na kufanya jitihada zote hizo wanapaswa kufanya kazi ya ziada kuhakikisha magari yanapanda katika ule mlima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali yangu mawili ya nyongeza ambayo nilitaka Mheshimiwa Waziri aweze kunijibu. Kuna Barabara ya Kanga – Ifwekenya haijalimwa muda mrefu. Nilitaka kufahamu ni lini Serikali itailima barabara hii na kuiweka kuwa kwenye kiwango cha kokoto?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Barabara ya Mlowo – NAFCO – Magamba ambayo inaunganisha Wilaya ya Songwe na Makao Makuu ya Mkoa. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha barabara hii inaweza kupitika muda wote na kutengenezwa kiwango cha lami ili iweze kuunganisha Mkoa wa Songwe? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwandabila, la kwanza juu ya hii Barabara ya Kanga hadi Ifwekenya. Barabara hii ina urefu wa kilometa 20.4 na tayari Serikali kutoka mwaka wa fedha 2021/2022 ilianza kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa maeneo korofi ya barabara hii. Mwaka wa fedha huo nilioutaja, Serikali ilitenga Shilingi milioni 250 kwa ajili ya ukarabati na hivi sasa kuna fedha nyingine katika mwaka wa fedha tunaomaliza, ilitengwa kwa ajili ya ukarabati wa kilometa saba kwa barabara hii ya Kanga kwenda Ifwekenya. Mwaka wa fedha tunaoenda kuanza Julai mosi 2023/2025 kuna Shilingi milioni 60 ambayo imetengwa kwa ajili ya ukarabati wa barabara hii. Serikali itaendelea kukarabati barabara hii kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha kuhakikisha kwamba huduma kwa wananchi zinapatikana muda wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili kuhusu barabara hii ya Mlowo – NAFCO, nikiri kwamba ni barabara muhimu sana ambayo inaunganisha Wilaya ya Songwe na Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe pale Mlowo. Barabara hii imetengewa fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida. Kwa sababu barabara hii pia na yenyewe haipo katika kiwango cha changarawe, kwa hiyo, katika mwaka wa fedha unaoanza wataanza ukarabati katika maeneo korofi kuweka changarawe badala tu ya kuwa wameilima na greda, wataanza kuweka kifusi katika maeneo korofi na tutaendelea kuitengea fedha kadiri ya miaka ya fedha inavyokwenda na upatikanaji wake.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Ikana – Chitete pamoja na kujenga kwa kiwango cha lami barabara za milimani?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Ni kweli tulitengewa fedha, Shilingi bilioni moja kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amejibu kwenye maswali yangu ya msingi. Barabara hii ya Ikana – Chitete ni barabara ambayo inaunganisha Tarafa ya Ndalambo pamoja na Tarafa ya Msangano ambapo Tarafa ya Ndalambo ndiyo kuna soko la kimataifa. Shilingi milioni 400 ambazo tumetenga kwa sasa haziwezi kushusha ule mlima; je, Serikali haioni kupitia Wizara ya TAMISEMI angalau mtuongezee shilingi milioni 600 nyingine ili tuweze kushusha ule mlima kikamilifu kama ambavyo Mlima wa Jimbo la Kwela unapitika? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge, jiografia ya kule na kuna mito mingi kwa ajili ya kueleka katika Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya hii ya Momba kule Chitete na inaunganisha pia tarafa hizi mbili ya Ndalambo na Msangano. Kama nilivyokuwa nimeshasema kwenye majibu yangu ya msingi, tayari Serikali ilikuwa imeanza ukarabati wa njia hii katika yale maeneo ambayo yalikuwa ni korofi sana. Tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuona ni namna gani tunaweza tukaongeza nguvu kwa ajili ya kuongeza ukarabati wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari kuna maeneo ambayo mto unapita ukitoka juu kwa sababu tunapozungumzia ni chini na unatakiwa upite kwenda kupanda mlima mrefu sana na kukutana na barabara ya Zambia. Tayari Serikali ilikuwa imeshaanza ukarabati wa vivuko vile katika maeneo ambayo maji pia yanapita. Kwa hiyo, tutakaa na Mheshimiwa Condester kuweza kuona ni namna gani tunaendelea na ukarabati huu. (Makofi)