Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, lini barabara ya Irambo - Nsonyanga ambayo inaunganisha barabara ya Isyonje – Makete hadi Njombe na TANZAM itapandishwa hadhi?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naishukuru Serikali Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi alisharidhia kupandisha hadhi hiyo barabara kuwa ya Mkoa. Kwa vile hii barabara iko kwenye hali mbaya sana.

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hii barabara ili ianze kupitika?

Swali la pili, katika hali hiyo hiyo kuna barabara ya Ilembo - Isonso ambayo inaunganisha Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe. Je, ni lini hii barabara nayo itapandishwa hadhi kuwa ya Mkoa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Njeza kwanza lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii ambayo tayari imeshapandishwa hadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, barabara ikiwa imeshakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi na ikapandishwa hadhi na kuwa inahudumiwa na TANROADS basi ni wajibu wa TANROADS kutenga bajeti hiyo kuweza kutengeneza barabara. Tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi na kuona wao wamejipanga vipi kwa ajili ya kutengeneza barabara hii ambayo ni muhimu sana kule Jimboni kwa Mheshimiwa Njeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la barabara ya Ilembo-Isonso ambayo inaunganisha Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Songwe lakini hasa katika Wilaya ya Ileje. Barabara hii itapandishwa hadhi pale ambapo watafuata vile vigezo vya kisheria kama ambavyo barabara nyingine zinafanya. Waanze vikao vyao katika DCC waende kwenye RCC na baadaye Bodi ya Barabara ya Mkoa na kisha kumwandikia Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi mwenye dhamana ya barabara hizi za Mkoa, ili timu iweze kutumwa kwenda kwenye barabara hii ya Ilembo - Isonso, kufanya tathmini na kisha kumshauri Waziri wa Ujenzi kuhusu barabara hii kupandishwa hadhi.