Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Lagana, Itilima na Bunambiyu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, naomba niishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri, lakini bado kasi ya utekelezaji wa miradi inakwenda taratibu sana. Swali la kwanza: Je, Mheshimiwa Waziri, uko tayari kuambatana nami ili twende jimboni ili tukasukume kwa pamoja utekelezaji wa miradi hii katika jimbo langu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kata ya Bunambiyu pamoja na Mwasubi ni maeneo ambayo zikinyesha mvua huwa hayapitiki ni maeneo ambayo yanapata maji kwa wingi sana. Sasa, mko tayari kuhakikisha kwamba mnaweka msukumo mkubwa ili maeneo hayo yapewe kipaumbele, wakati huo huo maeneo hayo niliyoyataja na yenyewe yaweze kufanyiwa kazi kwa haraka?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Boniphace, amekuwa akifuatilia sana haya maeneo na mradi ule mkubwa wa umeme wa kutumia solar ambao tumeufanikisha juzi kuusaini, na katika Jimbo lake, mkoa wote wa Shinyanga na nchi nzima itakuwa ni faraja kubwa.

Mheshimiwa Spika, namuahidi kwamba niko tayari kuambatana naye kwenda kuhakikisha tunaendelea kumsimamia mkandarasi huyu kama tulivyoahidi katika bajeti. Vile vile, mbinu za kufungua LC, kuongeza wasimamizi na kuwawezesha, zitatusaidia kuhakikisha kwamba ndani ya muda tunakamilisha kazi hii. Hilo jambo la maeneo ambayo yana changamoto, tutalichukua kwa ukubwa wake ili kuhakikisha tunamaliza kazi hii mapema kwa mujibu wa mkataba. (Makofi)