Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza:- Je, ahadi ya Serikali ya kusambaza umeme wa REA III katika vijiji 48 vya Jimbo la Same Magharibi na vitongoji vyake imefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, tuna vijiji zaidi ya hivyo ambavyo amevitaja Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa mfano vijiji vya Gundusini, Mabilioni, Gavao, Saweni, Rwinndini, Ruvu, Jiungeni, Mferejini, Duma, Emugule na Endevesi vyote hivi havina umeme. Sasa Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari tutembelee vijiji hivi ili aone hali halisi kuliko kwamba zinawekwa nyumba mbili halafu tunaambiwa Kijiji kimewekewa umeme? Hilo halitakubalika.

Mheshimiwa Spika, la pili. Je, Serikali iko tayari kutoa kwa Wabunge orodha ya Wakandarasi wale wanaokwenda kuweka umeme katika maeneo yao ili nao waweze kufuatilia? Ahsante sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru Waheshimiwa Wabunge jana wametupitishia bajeti kwa ajili ya kwenda kutekeleza miradi na ahadi ambazo tumezitoa. Pia nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari kuambatana naye kwenda jimboni kwake baada ya Bunge kuisha ili kuona vijiji hivyo ambavyo havijafikiwa na umeme. Kama tulivyosema viko tisa na ni kweli hata jana tumesoma kwenye bajeti, tunatambua kwamba sio wananchi wote na vitongoji vyote vimepata umeme, lakini jitihada na hatua zimeanza na tunaamini tutakamilisha. Ifikapo Desemba, 2023 hatutarajii kuwa na kijiji ambacho hakijafikiwa na miundombinu ya umeme.

Mheshimiwa Spika, katika eneo lingine, tuko tayari na tulishafanya hivyo na tutafanya tena kuhakikisha kila Mbunge anamfahamu Mkandarasi wake na scope yake na wale wanaosaidia katika usimamizi. Nikitoka hapa nitapitia kwa Mheshimiwa Mbunge nimpatie pia wale wa kwake wanaofanya kazi kwenye maeneo yake ili aweze kuwa na nafasi nzuri ya kufanya ufuatiliaji yeye mwenyewe.