Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni ni kwa nini Serikali pindi inapotwaa maeneo ya wakulima isiwatengee maeneo mengine mbali ya kulipa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza, kwa vile kumekuwa na malamaiko ya wananchi ambao wananyang’anywa mashamba yao halafu wanapewa hela. Katika harakati za kuhangaika kutafuta mashamba mpaka ile hela inaisha. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kuelimisha wananchi kuhusu Sheria hii ili pale wanapopewa fedha waombe pia wapewe na shamba?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kutokana na kwamba ardhi kubwa ya Tanzania haijapimwa. Je, Serikali itakapowapa mashamba mbadala hawa wananchi walionyang’anywa itawahahikishiaje kwamba hawatahamishwa tena maana haya yameshatokea na wananchi wanahangaika sana katika kuji-establish mara ya tatu. Naomba nipate majibu.

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa swali lake la kwanza kwamba tutoe elimu ya hii Sheria kwa wananchi ili waweze kupata fidia zote mbili kwa pamoja au kwa namna yoyote ile.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, suala la fidia linazingatia sana mazingira ya eneo ambapo mtu anafidiwa. Kwa hao wenzetu wa kulima kimsingi mamlaka za Mkoa huwa zinashirikishwa kwa karibu sana katika suala zima la namna ya kuwapa fidia ya maeneo mengine wale wananchi na kumekuwa hakuna matatizo makubwa sana. Usalama wa mashamba pale wanapofidiwa yale mashamba kwa vyovyote kama ni mkono wa Serikali umekwenda kuwaondoa pale. Yale mashamba mapya watakayopewa lazima yatolewe kwa utaratibu wa kupimwa na wapewe zile hati ambazo zitawasaidia kuwaweka kwenye usalama wa maeneo mapya waliyopewa.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni ni kwa nini Serikali pindi inapotwaa maeneo ya wakulima isiwatengee maeneo mengine mbali ya kulipa fidia?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwenye Jimbo langu eneo la Mgodi wa Barrick North Mara, Serikali ilipeleka Mthamini Mkuu wa Serikali ikafanye evaluation eneo la kiwanja na Mkomalela North tangu mwaka jana. Mwaka huu wanasema hawana mpango wa kutoa hilo eneo.

Je, nini kauli ya Serikali kwa wananchi wale katika maeneo ya kiwanja na Mkomalela?

SPIKA: Swali hilo nadhani limeshawahi kujibiwa na Wizara ya Madini ama sio swali hilo. Mheshimiwa Waitara ni swali hilo hilo au sio.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ule mgogoro upo huu wamezua mwingine juzi tena hili ni jipya. Ni jipya kabisa.

SPIKA: Ambaye hana mpango wa kuchukua ni nani? Mgodi.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, yaani Mgodi ili ulipe fidia Wizara ya Ardhi inatuma Mtathmini anafanya tathmini walifanya hivyo na wakatoa notice kuzuia wanainchi wasiendeleze maeneo yale kwa sababu mgodi unachukua. Baada ya mwaka mmoja. Juzi madiwani na wenyeviti wa vijiji wakaitwa eneo hilo wakaambiwa sasa mgodi hauna mpango wa kutwaa hilo eneo, shida inabaki hapo.

SPIKA: Nataka kuelewa ni swali hilo hilo ambalo limewahi kujibiwa na Madini kwa sababu Serikali ni moja asije huyu wa ardhi hapa akajibu tofauti na wale wa madini halafu tukatekeleza mgogoro mwingine. Wewe niambie ni swali hilo hilo ambalo umeshawahi kuuliza kwa Wizara ya Madini au hapana.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ni swali jipya kama hana majibu anaweza akajipanga. Mimi nitali...

SPIKA: Hapana, yeye sijampa nafasi ya kujibu bado nataka tuelewani mimi na wewe kwanza ili nijue nimpe nafasi yupi maana Serikali ni moja. Swali ni hilo hilo au ni tofauti.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ni swali jipya, ahsante.

SPIKA: Kuhusu jambo hilo hilo.

MHE. MWITA M. WAITARA: Ndio, jambo hilo hilo.

SPIKA: Swali jipya kuhusu jambo hilo hilo.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ndio.

SPIKA: Watu wa Madini, Waziri.

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, swali alilozungumza Mheshimiwa Waitara na hata tulivyojibu wakati ule, tulikuwa tunazungumzia eneo la Mrwambe na Nyamichune. Maeneo ambayo yalifanyiwa uthamini baadae mgodi ukaonesha kwamba hauyahitaji ukawarudishia wananchi. Sasa kwa sababu wananchi walikuwa wamesubiri kwa muda na kwa mujibu wa Sheria ikabidi walipwe kitu kinachoitwa fedha ya usumbufu au excrasher. Kwa hiyo, mwezi wa sita huu mgodi umeshakubali kulipa hizo fedha na Mheshimiwa Waitara tulishazungumza. Namuomba tu avumilie kidogo kwa sababu mwezi wa sita ndio huu tumeuanza watalipwa wakamilishe.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Je, ni ni kwa nini Serikali pindi inapotwaa maeneo ya wakulima isiwatengee maeneo mengine mbali ya kulipa fidia?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Nilitaka kujua ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa shamba la EFATHA ambalo unavikumba vijiji vya Msanda, Muungano, Kaungu, Sandulula, Malonje, Ulinzi na Mawenzusi. Ni lini sasa mgogoro huu utaisha wananchi wanapata tabu sana sana hawana pa kulima. Tunaomba Serikali imalize mgogoro huu. Ni lini sasa Serikali itamaliza mgogoro huu? Ahsante.(Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza Waheshimiwa Wabunge ni wape angalizo. Vyanzo vingi vya migogoro ni matumizi ya nguvu yasiyozingatia utaratibu. Tunapotoa shamba kwa mwekezaji, mwananchi mwingine yeyote haruhusiwi kwenda kulivamia lile shamba bila kuzingatia taratibu. Kama unaona kabisa kwamba zile taratibu za umiliki wa yule mmiliki zimekiukwa fuata taratibu tulishatoa maelekezo. Halmashauri zianzishe ule mchakato wa kumjadili huyu muhusika wa shamba hilo ambaye amelitelekeza.

Mheshimiwa Spika, wananchi kuanza kuvamia maeneo haya kwa kweli sio kitu cha busara sana. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge sisi ni viongozi wote tushirikiane kwenye hili kuwaelimisha wananchi juu ya taratibu zinazoweza zikafatwa ili kupata kile ambacho tunakihitaji kwa matumizi yetu.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri anataka kujua mgogoro utamalizwa lini maana yake mgogoro upo wewe umeelezea kuzalishwa kwa mgogoro sasa kwa kuwa mgogoro tayari upo utakwisha lini ndio swali la Mbunge.(Makofi)

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kusema maelezo haya tayari tumekwishaanza na tumeunda timu ya ufatiliaji ili makundi ya pande mbili zote yakutane ili kuona uwekezekano wa kulimaliza hili tatizo.

Mheshimiwa Spika, kama mninavyosema vyanzo vikubwa vya migogoro hii ni matumizi ya nguvu zisizozingatia taratibu.

SPIKA: Hilo umeshaeleweka, hoja ni kwamba mgogoro ukisha kuwepo lazima umalizwe, lazima umalizwe. Ukishakuwepo mgogoro umeshatengenezwa lazima umalizwe sasa aliyepelekea huko. Naona Waziri amesimama.

Mheshimiwa Waziri.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa fursa kwa ajili ya kujibu suala hili na nimshukuru pia Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.

Mheshimiwa Spika, mgogoro huu wa EFATHA na wananchi wa Sumbawanga kama alivyosema. Mgogoro huu ni wa siku nyingi na mgogoro ulisha wahi kufika mahakamani lakini ulitokana pia na mgawanyo wa maeneo katika lile eneo ambapo mwekezaji alipewa. Mwekezaji alifata taratibu zote katika kupewa yale maeneo. Changamoto inapokuja ni kwamba kadri mahitaji ya wananchi yanavyozidi kuwa makubwa basi wanaona kama vile mwekezaji pengine amekiuka taratibu katika kupewa, lakini taratibu zote zifuatwa.

Mheshimiwa Spika, naomba niwahakikishie wananchi wa Jimbo la Sumbawanga ambako ndiko kuna mgogoro huo, nitakwenda mwenyewe kule kwa ajili ya kuzungumza nao ili tuweze kuumaliza kwa sababu umekuwa ni wa muda mrefu. Tutapanga na Mbunge kwenda kuumaliza mgogoro huo. (Makofi)