Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR aliuliza: - Je, kwa nini Serikali haipangi kusahihishia mitihani ya kidato cha nne Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Ni masomo gani ambayo yalisahihishwa katika kipindi hicho alichokitaja Mheshimiwa Waziri 2021/ 2022?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, Wizara imejipanga kusahihisha mitihani mingapi katika mwaka 2023?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ali Omar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika utaratibu wa usahihishaji wa mitihani kila kituo kawaida huwa kina sahihisha mtihani mmoja na kwa miaka hiyo niliyoitaja ya 2021/2022 katika kituo hiki cha Zanzibar ni somo la civics ndilo ambalo lilisahihishwa katika kituo hicho.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anataka kufahamu ni mitihani gani ambayo itasahihishwa. Masuala ya mitihani na masomo gani yatasahihishwa ni jambo la siri. Kwa hiyo, hatuwezi ku-disclose hatuwezi kufungua hapa sasa hivi ni mitihani gani utakwenda kusahihishwa kwenye kituo hiki na ni mapema Sana.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tarehe 26 Juni, tutaanza kufanya ukaguzi wa vile vituo ambavyo tunalenga sasa mitihani itakwenda kusahihishwa lakini somo gani kwamba linapelekwa katika kituo hicho litaendelea kuwa siri mpaka baada ya kazi hiyo kumalizika, nakushukuru sana.