Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha matawi ya Vyuo Vikuu vya Umma katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa ni azma ya Serikali kukuza kilimo nchini. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuwapa kipaumbele kwenye mikopo wanafunzi ambao wanachaguliwa kwenda kusomea masomo ya kilimo hususan katika kampasi zilizopo pembezoni mfano kampasi ya Mizengopinda ya sasa hivi ina zaidi ya miaka mitatu ambayo imejikita zaidi katika kutoa elimu ya nyuki?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa sasa katika Mkoa wa Katavi tuna hiyo kampasi moja. Serikali haioni kuna umuhimu wa kuongeza kamapasi nyingine ili kupanua wigo wa elimu katika Mkoa wetu wa Katavi kwa kuongeza kampasi kama vyuo vya afya pamoja na vyuo vya uhasibu? Nakushukuru.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha Mariki Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwenye swali lake la kwanza anataka kufahamu mkakati wa Serikali juu ya mikopo. Naomba kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge Serikali imekuwa ikiongeza kiwango au kiasi cha mikopo kwa wananfunzi wa elimu ya juu. Kwa takwimu zilizopo kwa mwaka 2021/2022 tulitenga na kupeleka jumla ya bilioni 570 kwa ajili ya wanafunzi hao. Mwaka 2022/2023 tulipeleka zaidi ya bilioni 554 hela ya kawaida lakini tulikuwa na vile vile bilioni tatu kwa ajili ya Samia Scholarship lakini katika bajeti yetu vile vile tumeweza kutenga jumla ya bilioni 738 kwa ajili ya mikopo katika mwaka ujao wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote kwamba Serikali imejipanga na kujizatiti kuhakikisha kwamba wanafunzi wetu wanapata mikopo kwa wakati wake.

Mheshimiwa Spika, tuna kozi za vipaumbele ikiwemo na hiyo aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge kozi za sayansi lakini zile za uhandishi, kozi za udaktari na kozi hizi za kilimo pamoja na masuala ya nyuki kwa ujumla wake ndizo ambazo tunazizingatia katika utoaji wa mikopo katika kipindi kijacho.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anataka kufahamu utaratibu gani Serikali itatumia kuongeza idadi ya vyuo. Nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge. Uwepo wa kampasi hii unaweza ukasaidia katika kuongeza aidha ndaki au shule nyingine katika kampasi hii. Kwa sababu tukumbuke hata hiyo University of Dar es Salaam wakati inaanzishwa ilianza na kozi moja lakini imeweza kupanuka mpaka hivi sasa ina kozi mbalimbali. Kwa hiyo, hata kozi hizi hapo baadae tutaangalia uhitaji na namna gani ya kuweza kuangalia kozi nyingine za kuanzishwa katika kampasi hii, nakushukuru.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha matawi ya Vyuo Vikuu vya Umma katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuzingatia kwamba Mkoa wa Songwe ni mpya naomba kufahamu Serikali ina mkakati gani wa kutujengea angalau kampasi moja tu ya chuo kikuu cha umma, ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shonza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza katika majibu ya swali la msingi kwamba tunakwenda kujenga kampasi 14 katika mikoa kumi na nne nchini. Moja ya Mikoa ambayo tunaweza kujenga ni katika Mkoa wa Songwe ambapo Chuo chetu cha DIT ndicho ambacho kitakwenda kujengwa katika eneo hili la Songwe.

Mheshimiwa Spika, kwa ruhusa yako labda ningeweza kusema na mikoa mingine ambayo inaweza kujengewa ili Waheshimiwa Wabunge waweze kujua. Naanza na Mkoa wa Manyara Chuo chetu cha TIA kitakwenda kujenga tawi pale. Singida ni TIA, Kagera University of Dar es Salaam, Lindi University of Dar es Salaam, Ruvuma ni TIA, Shinyanga ni MAMCU, Simiyu ni IFM, Rukwa ni MUST, Tabora ni Julius Nyerere, Kigoma ni MUHAS, Zanzibar ni University of Dar es Salaam, Mwanza ni ARU, Tanga ni Mzumbe na Songwe ni DIT, nakushukuru.