Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, kwa kiasi gani Mkongo wa Taifa umesaidia kuboresha na kupunguza gharama za mawasiliano?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, ili upitishe miundombinu ya mawasiliano kwa kila kilometa moja watu wa mawasiliano wanachajiwa dola 1,000, lakini ukipitisha miundombinu kama ya maji au umeme kando ya barabara kuu za TANROADS au za TARURA, charge yake ni kama dola 50 kwa kilometa moja.

Je, Serikali haioni ni wakati sasa wa kuzungumza ndani kwa ndani ya Serikali ili kupunguza hiyo gharama ya dola 1,000 ili kupunguza hizo gharama za mawasiliano?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; maeneo ya Mtula, Kisada na Kata nzima ya Bumilayinga, kuna masiliano ya kusuasua: -

Je, ni lini Serikali itaboresha na kuimarisha mawasiliano katika kata hizo za Mji wa Mafinga?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweIi kabisa kuna gharama za kupitisha mkongo wa Taifa ambazo ni dola 1,000 ambazo tunaziita right of ways na Mheshimiwa Rais tayari ameshaelekeza tuhakikishe kwamba tunalifanyia kazi kwa sababu gharama hizi mwisho wa siku zinaingia kwenye capex na mwisho wa siku zinaenda kwa mtumiaji wa mwisho.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ili tuhakikishe kwamba mtumiaji wa mwisho anapata huduma ya mawasiliano kwa gharama nafuu ni kuhakikisha kwamba gharama ambazo zilizopo katikati hapa ambazo zitamsababishia mtumiaji wa mwisho kuwa na gharama kubwa ya kutumia huduma ya mawasiliano tumeshaanza kazi nzuri ya kushirikiana na wenzetu TANROADS, TARURA na kadhalika ili kuhakikisha kwamba hizi gharama tumezitazama kwa namna ambayo zitasaidia zaidi wananchi badala ya kuwaumiza wananchi, ahsante sana.