Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 1

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ninataka niulize swali moja la nyongeza kwa Serikali: -

Jimbo la Songwe ni jimbo ambalo liko kijijini sana, na Kata za Magamba, Mpona, Ifwenkenya, Manda, Mkukwe, Ngwara na Gua hazina mawasiliano kabisa;

Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika kata hizo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Phillipo Augustino Mulugo, Mbunge wa Jimbo la Songwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimesema, ili vijiji viingizwe katika utekelezaji ni lazima kwanza vifanyiwe tathmini, na tayari katika vile vijiji 2,116, vijiji vya Mkoa wote wa Songwe vipo. Na juzi tumesaini mikataba ya kupeleka minara 758 lakini Mheshimiwa Rais ametafuta fedha kwa ajili ya minara mingine 600. Kwa hiyo naamini kwamba katika vijiji ambavyo tayari vimeshafanyiwa tathmini, tutapeleka minara hiyo 600 ili kuhakikisha kwamba huduma ya mawasiliano inaimarika kwa wananchi.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninataka kujua tu, kwanza ni lini vijiji hivyo vitafanyiwa tathmini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pale Singida Mjini, Kata ya Unyamikumbi ndiyo kata pekee ambayo mawasiliano yanasumbua sana: -

Je, ni lini Serikali itatuletea mnara kwa ajili ya kutatua tatizo la mawasiliano katika kata ile?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mussa Ramadhani Sima kwa niaba ya Mheshimiwa Katani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini tayari imeshaanza kufanyika na awamu ya kwanza tumekamilisha vijiji 2,116. Kwa hiyo naamini kwamba katika awamu ijayo vijiji na kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti zitaingizwa katika utekelezaji huo, na baada ya hapo, fedha zitakapopatikana tutafikisha huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kipengele cha pili kuhusu Kata ya Singida Mjini pale, tutatuma wataalam wetu wakaangalie tatizo ni lipi hasa. Kama ni kuongeza nguvu tutafanya hivyo, na kama itahitaji kupeleka mnara tutafanya hivyo. Ahsante sana.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Vijiji vya Kapewa na Mtetezi vilivyopo Kata ya Mpui vina changamoto kubwa ya mawasiliano. Nataka kujua ni lini Serikali mtapeleka minara katika vijiji hivyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, vijiji ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja vipo katika utekelezaji wa Mradi wa Tanzania Kidigitali. Ahsante sana.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza; je, ni lini Serikali itapeleka mtandao katika Vijiji vya Hunyali, Kihumbu na Sarakwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge tayari ameshafika ofisini kwetu na mimi nimekuwa nikiwasiliana naye mara kwa mara na tayari vijiji ambavyo ameshavileta ofisini viko kwenye mchakato wa kuingizwa katika utekelezaji. Pindi fedha zitakapopatikana tutafikisha huduma ya mawasiliano katika vijiji ambavyo Mheshimiwa Getere amevitaja.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 5

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano katika Kata ambazo Jimbo la Tabora Kaskazini hakuna mawasiliano; Igulungu, Chitage, Bukumbi na Chese?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa, tunakiri kwamba Tabora Kaskazini ina changamoto kubwa sana ya mawasiliano; na katika mradi wetu huu kwa bahati mbaya sana haikuwezekana. Hata hivyo, tayari tumeshachukua kata tano za Tabora Kaskazini ambazo tunakwenda kuzifikishia huduma ya mawasiliano ndani ya mwaka huu wa fedha, ahsante sana.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu yenye usikivu katika Kata za Litehu, Ngonja na Mkwiti Wilayani Tandahimba?

Supplementary Question 6

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli kabisa Dar es Salaam, hasa Dar es Salaam Vijijini, Kibamba kule, mawasiliano ni shida. Maeneo ya Mabwepande eneo la Kibesa na maeneo ya Kata ya Saranga, maeneo ya mpakani na Ilala hakuna kabisa mawasiliano: -

Je, Serikali mko tayari kwa minara 600 hii kupeleka na maeneo hayo? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge wiki jana alinifikishia changamoto hii, na tayari Serikali tumeshaipokea na tunaifanyia kazi. Tutamjulisha Mheshimiwa Mbunge hatua ambayo tutakuwa tumefikia kulingana na upatikanaji wa fedha.