Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mbalizi – Shigamba, ile barabara ni muhimu sana, ambayo inaunganisha na Mkoa wa Songwe;

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; hili swali linajirudiarudia lakini halijapata majibu sahihi ya Serikali; barabara ya kutoka Katumba – Suma – Mwakaleli – Luangwa – Mbambo na Tukuyu Mjini, hii ni ahadi ya tangu awamu ya nne;

Je, ni lini Serikali itaanza kuijenga barabara hiyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbalizi – Shigamba tayari tulishapata maelekezo na tunaifanyia kazi. Hivi sasa tunakamilisha usanifu wa kina na mhandisi mshauri yupo kazini. Akishakamilisha barabara hii ambayo ni ya Mbalizi – Shigamba na inaunganisha Itumba na Malawi, sasa Serikali itaanza kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, na barabara ya pili aliyoitaja, kimsingi tumeshaitengea fedha kwa kipande kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Njombe – Mdandu – Iyai kutokea Mbeya kwa kuwa barabara hii ni muhimu ndani ya Jimbo la Wanging’ombe na hatuna barabara ya lami yoyote zaidi ya hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara inayoanzia Njombe – Ramadhani – Iyai, Serikali imekuwa inajenga kwa awamu. Na katika mwaka huu wa fedha nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tumetenga fedha kwa ajili ya kuendelea kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami kuunganisha Makao Makuu ya Wanging’ombe na Makao Makuu ya Mkoa wa Njombe.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kuuliza Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo barabara ya ulinzi ya Kusini sehemu ya Kivava – Kitaya baada ya mafuriko yaliyotokea hivi karibuni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya vipaumbele vya Serikali ni kuhakikisha kwamba barabara zote za ulinzi zinapitika. Barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge bado ni barabara ya changarawe, na kutokana na mvua iliyonyesha kama alivyosema, kuna maeneo ambayo hayapitiki.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tayari imeshaanza kufanya mipango ya kurudisha mawasiliano maeneo yote yaliyokatika ili iweze kupitika, hasa tukizingatia umuhimu wa barabara yenyewe, barabara ya ulinzi, ahsante.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Bukonyo – Bukongo – Masonga yenye kilometa 32 kwa sababu upembuzi yakinifu ulikwisha fanyika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Ntengo Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge itajengwa baada ya kufanya usanifu wa kina wa mwisho ambapo ile barabara bado hatujafanya usanifu. Kwa hiyo tukishafanya usanifu tutajua gharama na ndipo Serikali sasa itatafuta fedha kujenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, lini barabara ya Makongolosi – Mkiwa – Chunya itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Namanyere – Kipili Port ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Wilaya ya Nkasi na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla;

Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mbunge barabara hii inakwenda kwenye Bandari ya Kipili. Tumetenga fedha kiasi kwa ajili ya kuifanyia ukarabati mkubwa ili iweze kupitika. Lakini lengo la Serikali ni kuijenga hii barabara kwa kiwango cha lami, hasa tukizingatia umuhimu wenyewe, kwamba inakwenda kwenye bandari ambayo inahusisha biashara kati ya Tanzania na DR Congo. Ahsante.