Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itaboresha Madaraja ya Kampimbi na Mgandu Wilayani Same?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naishukuru Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Sita kwa kuiona barabara ile kwa kuwa imekuwa na changamoto kubwa sana. Naishukuru Serikali kwa kuingia mkataba wa kutengeneza barabara ile ya Mkomazi – Kisiwani – Same. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja tu la nyongeza. Kuna maeneo ambayo yalitengenezwa kwa kiwango cha lami, kilometa tano, tatu na tano tena; katika Kata ya Ndungu zimetengenezwa kilometa tano, katika Kata ya Maore zimetengenezwa kilometa tano na katika Kata ya Kihurio zimetengenezwa pia kilometa tano…

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa.

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Je, Serikali sasa kupitia mkataba huu itabomoa ile lami ambayo imetengenezwa ambayo imeanza kuchakaa au itaendelea na ile ile? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Zuena Bushiri, Mbunge, Viti Maalum, Mkoa wa Kilimanjaro, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza napokea hizo pongezi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuhusu suala lake la maeneo ambayo tumeyajenga, wakati hizi barabara zinajengwa kwa vipande vipande yalikuwa ni maelekezo kutokana na wananchi wa maeneo hayo yalivyokuwa korofi, lakini pia kwenye miji midogo waliomba viongozi na wakatoa maelekezo barabara hizo ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami kwa vipande vipande.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na wananchi ambao wanahusika na hiyo barabara, usanifu uliofanyika, hayo maeneo yameshakuwa yamechakaa na hayaendani na usanifu wa sasa. Kwa hiyo, maeneo yote yale yatafumuliwa na yatajengwa upya, isipokuwa kuna kilometa tano na kitu ambayo inaendela kujengwa, hiyo ndiyo ianendana na usanifu wa sasa, lakini maeneo yote ya zamani yatafumuliwa na kujengwa upya, ahsante.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itaboresha Madaraja ya Kampimbi na Mgandu Wilayani Same?

Supplementary Question 2

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Barabara ya Tengeru – Holili itaanza kupanuliwa ikiwa ni pamoja na kujenga daraja jipya la Kikavu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja pamoja na daraja hilo, tayari yapo mazungumzo, na JICA wameshakubali kufadhili ujenzi wa barabara hiyo na daraja hilo la Kikavu ikiwa ni pamoja na barabara kama kilometa 10 katika Mji wa Moshi. Kwa hiyo, sasa hivi suala linaloendelea ni mazungumzo kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na JICA ili tuanze kujenga hayo maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, ahsante. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itaboresha Madaraja ya Kampimbi na Mgandu Wilayani Same?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Barabara ya Mkomazi – Kisiwani – Same ni kweli ina madaraja mengi sana: Je, Mheshimiwa Waziri, Daraja la Saseni na Daraja la Mpirani, nayo mtayarudisha yawe mapya kama ambavyo barabara itakuwa mpya? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema, usanifu huu ni mpya tofauti na uliokuwepo zamani. Kwa hiyo kila kitakachofanyika ni kujenga barabara yote, hizo kilometa 98 ikiwa ni pamoja na hayo madaraja, ahsante. (Makofi)