Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:- Je, kuna mwongozo unaoruhusu watu wenye ulemavu mmoja mmoja kukopeshwa fedha za Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Serikali imetoa wito kwamba Wabunge tutoe elimu. Mimi kama Mbunge wa kundi hili, nimetoa elimu sana na kundi hili limekuwa likiitikia, lakini Halmashauri na Manispaa huwa hazitekelezi mwongozo huu na kanuni ambayo imeelezwa kwenye jibu la msingi: Nini kauli ya Serikali kwa Halmashauri na Manispaa zetu nchini? Kwa sababu kama mwongozo upo na kanuni zipo, kwa nini halitekelezeki? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba huenda kukawa kuna mabadiliko ya jinsi ya utolewaji wa mikopo hii. Niendelee kuiomba Serikali kwamba kwa kundi hili la watu wenye ulemavu, iendelee kufikiria kukopesheka mtu mmoja mmoja, ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Ikupa kwa maana amekuwa champion hasa katika mabadiliko ya kanuni hizi za kuwezesha walemavu kuweza kupata mkopo kwa mtu mmoja mmoja.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake kuhusu kwa nini kanuni hizi hazitekelezeki, nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kuwaelekeza Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini, kutekeleza mabadiliko haya ya sheria na kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata mkopo kwa mtu mmoja mmoja. Pia kama Mheshimiwa Ikupa alivyosema kwenye ushauri wake, katika mapitio mapya ambayo yanafanyika kwa maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutaweka kipaumbele kwenye kundi hili la walemavu vilevile kuweza kuendelea kupata mkopo mtu mmoja mmoja.