Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya marekebisho ya sheria zisizo rafiki kwa wavuvi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, ni lini tathmini hiyo itakamilika ili Watanzania wafanye kazi zao kwa ufasaha ili kuleta tija? Swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, kwa kuchelewesha kukamilisha taratibu hizo hatuoni kwamba tunawanyima Watanzania fursa katika kumiliki rasilimali zao? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi kwamba mchakato wa kubadilisha sheria ama kanuni ni mchakato unaofanyika mara kwa mara. Kama nilivyosema mwaka 2019 mchakato huo ulifanyika tukabadilisha sheria mbalimbali, mwaka 2020 tukabadilisha. Kwa hiyo, sheria ambazo zinaonekana pengine ni kandamizi kwa wadau wa uvuvi, Serikali iko tayari kuendelea kuzibadilisha mara kwa mara kadri ya mahitaji.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tathmini zinaendelea kulingana na sheria, jiografia na uhitaji wa maeneo husika. Lengo la Serikali hasa ni kuhakikisha kwamba sheria zinazotumika kumsaidia huyu mvuvi ama mtumizi wa sekta hiyo kurahisisha shughuli zake.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tathmini zinaendelea. Sheria ambazo ni kinzani na mahitaji ya watumiaji wetu, zinaendelea kubadilishwa siku hadi siku kama ambavyo zimekuwa zikibadilishwa mara kwa mara. Kwa hiyo, wataalamu wanaendele kufanya tathmini, lakini sio tu wataalam wa Wizara, ni pamoja na watumiaji wa sheria hizi wanaendelea kufanya tathmini siku hadi siku kama ambavyo sheria na kanuni zimekuwa zikibadilika, naomba kuwasilisha. (Mkofi)