Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR K.n.y. MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa madarasa na mabweni ya Chuo cha Usafirishaji (NIT) Mabibo?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Serikali nashukuru kwa majibu mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa chuo hichi cha usafirishaji kuongeza wanafunzi wa kigeni? Ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafirishaji ambacho kiko pale Dar es Salaam kina wanafunzi 14,464 na katika wanafunzi hao asilimia 99.2 ni wanafunzi wa Kitanzania na asilimia 0.8 ni wanafunzi wa nje.

Mheshimiwa Spika, chuo kimeendelea na programu mbalimbali za kuhakikisha kinaongeza wanafunzi wengi kama ambavyo imeulizwa na Mheshimiwa Mbunge ikiwa ni kwa ajili ya kuhakikisha tunaongeza forex, lakini pia kwa ajili ya kuongeza experience kwa wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Spika, programu mbalimbali zimefanyika katika chuo hicho ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Balozi zetu za nje kukitangaza chuo chetu kimataifa. Vile vile tumeshiriki katika mikutano mbalimbali mingine imefanyika Nchini Rwanda kwa ajili ya kuongeza na kutangaza chuo chetu.

Mheshimiwa Spika, kama hilo halitoshi, chuo chetu kwa sasa kinaandaa mkutano mkubwa tarehe 18 mpaka tarehe 20 mwezi ujao ambao ni First International Conference on Transport and Logistics and Management ili kuleta wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuhakikisha kwamba pengine tunaweza kujitangaza zaidi na kupata wanafunzi wengi zaidi, ahsante.