Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Je, lipi tamko la Serikali kwa watuhumiwa waliopo magereza ya nchi za nje wanaomiliki vitambulisho na hati za kusafiria za Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMARI KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nakubaliana na maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini napenda Watanzania wapatiwe elimu. Naomba kujua hiyo sheria inazunguza nini au inasema nini wakati kitendo kama hicho kikitokea ili Watanzania wote waelewe kwamba kuna sheria inazungumza hivi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa hicho kitendo sana huwa kinatokea nchi za nje na kule tuna balozi zetu. Je, balozi zetu zimepewa elimu gani kama litatokea tatizo kama hilo waweze kukabiliana nalo bila shida yoyote? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ikiwa aliyefanya kosa yuko Tanzania, sheria zinazopaswa kuchukuliwa ni pamoja na mhusika kufikishwa mahakamani kwa mujibu wa Sheria ya Pasipoti, Sheria ya Uhamiaji, Sura ya 54 iliyorejewa mwaka 2016. Baada ya kutiwa hatiani na kuadhibiwa hunyanganywa pasipoti ya Tanzania na kuifuta ili isije ikatumika tena. Jambo la tatu, hufukuzwa nchini kwa kupewa hati ya kufukuzwa nchini (prohibit legal notice) ili aondoke katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Maofisa wa Ubalozi wetu katika kila ubalozi tunaye Afisa Balozi ambaye ikitokea tutapata taarifa kama kuna Mtanzania kawekwa gerezani au kafungwa hufuatilia kumhoji ili kujua kama kweli ni Mtanzania na ikithibitika si Mtanzania, basi taarifa hutolewa kwenye nchi husika, lakini ikithibitika kwamba ni Mtanzania itabidi atumikie kifungo chake. Kitakachofanyika kama ni Mtanzania, atakuwa anakwenda kumsalimia, kumwona kwenye vile vipindi vinavyoruhusiwa na mambo kama hayo, nashukuru.