Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya polisi Moshi Manispaa?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi wa kuwakosoa au kuwasaidia wananchi hawa ambao ni Maaskari wetu wanaofanya kazi usiku na mchana ambao wanaishi katika mazingira magumu sana, kwa kuwa nyumba zao zinavuja na miundombinu imechoka sana?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana nami kwenda eneo la tukio akaone hali halisi ya makazi ya maaskari wetu wanavyoishi? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuena Athumani kuwa Serikali inatambua uchakavu wa Vituo vya Polisi lakini pia inatambua uchakavu wa nyumba za makazi kwa ajili ya askari hawa. Aidha, Serikali inatambua juhudi na kazi kubwa inayofanywa na Jeshi la Polisi katika ulinzi na usalama wa raia na mali zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie Mheshimiwa Mbunge, kwa sasa tunaenda kuzitafuta shilingi bilioni 3.6, zitakapopatikana tunaenda kuanza ujenzi wa nyumba hizo, lengo na madhumuni ni Askari wetu waweze kuishi kwenye mazingira mazuri. Aidha, nimwambie tu kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, tupo tayari kuambatana naye kwenda mpaka kwenye eneo ili kukagua na kuona uchakavu huo na kuona namna ya kuweza kuwasaidia, nakushukuru. (Makofi)

Name

Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya polisi Moshi Manispaa?

Supplementary Question 2

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nami naomba niulize swali la nyongeza. Katika Mkoa wetu wa Geita kuna nyumba nyingi sana za Askari ambazo ni chakavu; je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kukarabati nyumba hizo za askari ili askari wetu wa Mkoa wa Geita waweze kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rose, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema hapo awali kwamba kwa sasa Serikali tunatafuta fedha na zitakapopatikana, pamoja na maeneo mengine yenye uchakavu wa nyumba na vituo, tutahakikisha kwamba Mkoa wa Geita nao tunautazama, lengo na madhumuni sasa wananchi waweze kupatiwa huduma hizo vizuri zaidi, nakushukuru.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya polisi Moshi Manispaa?

Supplementary Question 3

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya makazi ya polisi katika Kituo Kikuu cha Iringa Mjini ni mbaya sana na majibu ya Naibu Waziri ni kwamba mpaka fedha zitafutwe. Nilitaka kujua wale askari wataendelea kuishi wapi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu la ulinzi na usalama katika Tanzania yetu ni jukumu la kila mtu na jukumu la kusaidia kuona kwamba huduma zinapatikana ni jukumu la Serikali lakini pia ni jukumu la viongozi. Namwomba basi angalau Mheshimiwa Mbunge naye aanze kuonesha mfano halafu sisi kama Serikali tutakuja kuongezea ili tuone namna ambavyo wananchi wanaweza kupata huduma hizo, nakushukuru. (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba za makazi ya polisi Moshi Manispaa?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Rungwe Tukuyu Mjini, hawana ukuta wa kutenganisha kituo cha polisi na shule ya msingi ili kuzuia watoto wadogo kuona jinsi wahalifu wanavyopelekwa kwenye kituo.

Je, ni lini Serikali mtawajengea ukuta wa kuzunguka ili waweze kuwa katika sehemu yao binafsi pekee kama polisi? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mara nyingi vituo hivi tunatakiwa tuviweke katika mazingira ambayo yanaweza pengine ingawaje vinatoa huduma kwa jamii, lakini jamii isiweze kuweza kuona mambo yanayoendelea pale lakini zaidi kuweza kukitengenezea mazingira ya usalama zaidi kile kituo. Nimwambie tu Mheshimiwa Sophia kwamba tunafanya juhudi za kutafuta fedha. Tutakapopata fedha hizo, tutakwenda kujenga uzio huo ili tuweze kutenganisha hayo maeneo, nakushukuru. (Makofi)