Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Je, ni minara mingapi ya mawasiliano ya simu itasimikwa Uyui kati ya minara 780 itakayojengwa nchi nzima?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na Serikali imetoa majibu mazuri sana, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; Kata ya Ibili ilikuwepo katika mradi wa kwanza ambao ulikuwa ujengewe mnara, je, imeondolewa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; wananchi wategemee lini mradi huu wa kata tano utaanza?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Ibili imo katika Mradi wa Tanzania ya Kidigitali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipengele cha pili, kama ambavyo nimesema katika jibu langu la msingi, Serikali kupitia UCSAF tunamtafuta mtoa huduma na mchakato utakapokamilika basi mtoa huduma atafika maeneo hayo kwa ajili ya kupata eneo na baadaye atapata vibali na kuanza shughuli ya ujenzi wa mnara huo kwa ajili ya wananchi wa Tabora Kaskazini. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Je, ni minara mingapi ya mawasiliano ya simu itasimikwa Uyui kati ya minara 780 itakayojengwa nchi nzima?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza namshukuru Naibu Waziri amefika kwenye jimbo langu. Je, minara ya Kata za Eshkesh, Endahagichan, Geterer, Maretadu, Gidarudagaw na Endamiley lini inajengwa?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mbulu Vijijini lipo katika minara 758 na tayari watoa huduma wapo katika hatua mbalimbali, hivyo nwmwomba Mheshimiwa Mbunge, wanapofika katika maeneo yake wananchi watoe ushirikiano kwa ajili ya kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa minara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, akishirikiana na watoa huduma, basi ujenzi wa minara utaanza mara moja. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Je, ni minara mingapi ya mawasiliano ya simu itasimikwa Uyui kati ya minara 780 itakayojengwa nchi nzima?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza. Kata ya Lihimalyao na Vijiji vyake vya Mangesani pamoja na Kisongo katika Jimbo la Kilwa Kusini, hakuna kabisa mawasiliano ya simu na katika awamu hii ya ujenzi wa minara 758 haijafikiriwa au haijapata nafasi. Nini mpango wa Serikali kwenda kujenga minara katika Kata ya Lihimalyao?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyaongea na inawezekana kuna maeneo mengine ndani ya nchi yetu bado hayajapa mawasiliano. Serikali inaendelea kutekeleza miradi hii kwa awamu. Awamu ya kwanza tumemaliza minara 758, kuna awamu inayokuja ambayo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametafuta fedha kwa ajili ya kuleta minara 600.

Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge, tukitoka hapa tukutane ili niweze kuchukua taarifa za uhakika kuhusu maeneo hayo ili tuwatume wataalam wetu, wakajiridhishe ili tuweze kuchukua hatua za kufikisha mawasiliano ndani ya kata hizo. Ahsante.