Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khamis Ali Vuai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkwajuni

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. ALI VUAI KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa maeneo hayo yaliyotajwa ni maeneo ya utalii na kumekuwa na matukio ya uhalifu; je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha ulinzi wa dharura ili kuwe na amani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa ujenzi wa nyumba na kituo cha polisi ni jukumu la Wizara; je, Serikali haioni haja ya kwenda kukaa na Serikali ya Mkoa, halmashauri na jimbo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusu umuhimu wa kuimarisha usalama kwenye eneo hili lenye watalii wengi, nitumie nafasi hii kumwekeleza IGP na hususani Kamishina wa Polisi Zanzibar kuimarisha huduma za doria ya magari ya askari wanaokwenda kwa miguu au pikipiki ili kuhakikisha wananchi na watalii wanaotembelea eneo hilo wanakuwa salama.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la kuimarisha ujenzi wa nyumba kupitia mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa (Halmashauri), hicho ndicho kipaumbele cha Wizara kwamba katika vituo vinavyojengwa hasa vile vidogo vya Daraja C ni jukumu la mamlaka zetu za Serikali za Mitaa ambazo ni moja ya kazi za msingi ya Serikali za Mitaa. Wizara imekuwa ikisaidiana na halmashauri hizi kukamilisha majengo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tuendelee kushirikiana kuzihamasihsa halmashauri hizi ili watimize huo wajibu wao nasi tutimize wajibu wa kujenga vituo vikubwa na ku–support vituo vidogo wanapokuwa wamefikia kiwango cha umaliziaji, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nataka kujua Serikali ina mpango gani wa dharura wa kuhakikisha kwamba inajenga vituo vya polisi vyenye hadhi ya kipolisi kwa Wilaya ya Tarime, Sirali, Nyamwaga na Utegi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli na Mheshimiwa Mbunge anatambua kwamba Mkoa wa Tarime – Rorya ni mkoa wa kipolisi, lakini kiutawala wako chini ya Mkuu wa Mkoa mmoja. Hata hivyo, tumeanza kutekeleza mpango wa ujenzi wa maeneo haya mapya. Ninatambua kwamba Jengo la RPC Tarime – Rorya almost limekamilika na sasa, tunakwenda kwenye ngazi ya Wilaya ili kujenga vituo vya ngazi ya Wilaya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa mujibu wa mpango wetu vituo vya Wilaya kwenye Wilaya mpya za kipolisi viko mbioni kwa mujibu wa utekelezaji wa mpango wetu wa miaka kumi. Nyamwaga na Sirali ni sehemu ya vituo vitakavyojengwa, nashukuru.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, wananchi wa Kata ya Bashnet tayari wametenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi; je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha polisi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kituo hiki kidogo cha Polisi cha Kata ya Bashnet ni kituo cha ngazi ya Daraja C. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge kupitia juhudi alizozifanya kama tulivyofungua kituo kipya hivi karibuni, alifanya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, waanze ujenzi kwenye eneo lao la Bashnet then Wizara kupitia Jeshi la Polisi itakamilisha mtakapokuwa mmefikia stage ya umaliziaji hasa lenta na uwekaji wa samani, nashukuru.

Name

Aloyce Andrew Kwezi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 4

MHE. ALOYCE A. KWEZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kupata ufafanuzi. Wilaya ya Kaliua hatuna ofisi ya OCD (jengo la polisi la Wilaya); je, Serikali iko tayari kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi ambapo pale Kaliua eneo lipo tayari?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kushirikiana na Wilaya ya Kaliua ili kuhakikisha kituo hicho kinajengwa. Kwa kuwa tayari wana eneo, tutawasiliana na IGP ili kwenye mpango wake wa miaka kumi wa kujenga vituo vya polisi ngazi ya Wilaya, Kaliua iweze kupewa kipaumbele pia.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?

Supplementary Question 5

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuishukuru Serikali kwa kutujengea Kituo cha Polisi Kata ya Songambele; je, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri tutakwenda pamoja Urambo ili ukatatue migogoro kati ya wananchi na Magereza ya Urambo?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: MMheshimiwa Spika, nimuombe mama yangu Mheshimiwa Margaret Sitta na nimuahidi kwamba wakati wowote nitakuwa tayari kuambatana naye. Tutaangalia ratiba yetu baada ya Bunge hili ili kwenda kuangalia tatizo lililopo kati ya wanachi na Gereza ili kupata suluhisho la kudumu, nashukuru.