Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa elimu kwa wafugaji kuhusu matumizi ya biogas ili kuhamasisha ufugaji wa kisasa?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Shirika la CARMATEC limebobea katika kutengeneza mitambo ya biogas; je, Serikali inajishughulishaje na shirika hili karika mambo ya utengenezaji wa biogas?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa nchi ya China inaongoza kwa uzalishaji wa biogas kwa kiwango cha cubic meters 15,000,000 kwa mwaka; je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka wananchi wetu wakasome wapate ujuzi wa hali ya juu wa kutengeneza biogas; kwanza kwa sababu tunahitaji kufuga zaidi kisasa kuliko kuswaga ng’ombe; na pili itapuguza uharibifu wa mazingira kwa ajili ya mmomonyoko wa udongo unaoletwa na ng’ombe wengi ambao wanachungwa badala ya kufungwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Mbunge anataka kujua namna ambavyo Serikali na Wizara yetu inavyoshirikiana na mashirika haya ikiwa ni pamoja na wadau wetu wa China. Wizara imepokea ushauri huo wa Mheshimiwa Mbunge. Tutakwenda kulifanyia kazi jambo hili la mashirikiano yetu na kupeleka wanafunzi wetu kwenda kujufunza nchini China.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, jambo hili tumelichukua na ushauri huu tumeupokea na tutakwenda kulifanyia kazi.