Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya Ajira ya Utumishi wa Umma kuongeza kigezo cha kujitolea ili kutoa fursa kwa wanaojitolea?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi na nashukuru kwa majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza, kwa kuwa kila kazi inayotangazwa tunaambiwa tunataka uzoefu na hakuna mtu anatoka shuleni na uzoefu. Kwa hivyo, walimu wanaojitolea hicho ni kigezo kwamba kujitolea sasa imefika wakati hii sheria iwe ni kigezo namba mbili baada ya meritocracy.

Swali la pili, kwa kuwa Wizara nyingi sasa zimeshatengeneza miongozo ya kujitolea, nilikuwa nasoma moongozo wa Wizara ya Elimu wa kujitolea kwa Walimu wa June na Wizara ya Maendeleo ya Jamii wa 2021, kwa nini sasa ninyi ambao ni wa Utumishi, muendelee kupoteza muda badala ya kuleta mabadiliko ya sheria haraka sana? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba iko miongozo mbalimbali ambayo inaongoza juu ya jambo zima la kujitolea, lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako kwamba maagizo yalikwishatolewa na Bunge lako juu ya Serikali kuanza utaratibu wa kuja na sheria na miongozo juu ya jambo la kujitolea kama nilivyoeleza katika jibu la msingi kwamba, kumekuwa na miongozo mbalimbali lakini hakuna utaratibu maalum unaolenga kuelekeza juu ya jambo zima la kujitolea.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako kwamba maagizo uliyoyatoa tunayafanyia kazi, na ndani ya Ofisi ya Rais – Utumishi, tumekwishaanza michakato hiyo na sasa hivi tuko katika document na kama nilivyoeleza kwamba document zitakapokuwa tayari tutazileta mbele ya Bunge lako Mheshimiwa Spika ili Wabunge waweze kutoa mawazo yao, baada ya hapo sasa tuweze kuleta ije kuwa sheria.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hilo pia nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako kwamba Serikali inayachukua mawazo yote mazuri yaliyotolewa na Wabunge, pamoja na michango yao katika kipindi cha Bunge la Bajeti na kwamba tunayafanyia kazi na kuyaleta mbele ya Bunge lako ikiwa kama miongozo ya Serikali.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya Ajira ya Utumishi wa Umma kuongeza kigezo cha kujitolea ili kutoa fursa kwa wanaojitolea?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa, wako watanzania wengi ambao wana ujuzi na stadi mbalimbali na ziko nchi ambazo tunapakana nazo zina uhaba wa kada mbalimbali za utumishi.

Je, Wizara hii iko tayari kuketi na Wizara ya Mambo ya Nje ili kuweza kuwasaidia Watanzania hawa waweze kupata ajira katika nchi hizo? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, wazo lililotolewa na Mheshimiwa Mbunge la kuketi na Wizara ya Mambo ya Nje, sisi kama Serikali niseme tunalichukua na tutakaa na wenzetu na kutengeneze miongozo mizuri ya kuona ni jinsi gani tunauza ajira nje ya nchi yetu.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya Ajira ya Utumishi wa Umma kuongeza kigezo cha kujitolea ili kutoa fursa kwa wanaojitolea?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, je, Serikali haioni uko umuhimu sasa wa kuweka majina ndani ya data base waliojitolea na wanaoendelea kujitolea ili wawe wa kwanza kuajiriwa wakati huo? Ahsante. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, hali ilivyo kwa sasa na miongozo iliyotolewa na Serikali inahifadhi majina ya watu wote wanaoshiriki michakato mbalimbali inayohusu ajira ndani ya database.

Mheshimiwa Spika, nataka nilihakikishie Bunge lako kwamba database tuliyonayo sasa inaishi kwa mwaka mmoja, baada ya mwaka mmoja ili turuhusu watu wengine nao waweze kuingia, lakini wazo analolisema ni moja ya mabadiliko makubwa ambayo yanakuja kuletwa na huu mchakato ambao sasa unafanyika wa mabadiliko ya Sheria ya Utumishi, pia sera mbalimbali zilizopo ili kuweza kuweka mahitaji yote ya ajira katika chombo kimoja lakini mwongozo mmoja ambao utaweza kutoa nafasi kwa Watanzania wote. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali italeta marekebisho ya Sheria ya Ajira ya Utumishi wa Umma kuongeza kigezo cha kujitolea ili kutoa fursa kwa wanaojitolea?

Supplementary Question 4

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika ahsante. Msingi wa kuanzishwa kwa mafunzo kwa vitendo kazini ni kuziba ombwe kati ya mafunzo waliyopata wahitimu vyuoni pamoja na soko la ajira. Sasa, kwa kutokuwa na kipaumbele cha kuajiri wale waliopata haya mafunzo kwa vitendo kazini kwanza, ni sawasawa na kupoteza lengo la kuanzishwa kwa mafunzo hayo. Sasa, kwa kutokuwa na kipaumbele cha kuajiri wale waliopata haya mafunzo kwa vitendo kazini kwanza, ni sawasawa na kupoteza lengo la kuanzishwa kwa mafunzo hayo? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Zainab Katimba niruhusu kidogo na mimi nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

SPIKA: Mheshimiwa Ridhiwani huko ni kupoka madaraka sasa, endelea (Kicheko)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nisamehe kwa sababu niliona kwamba niombe ruhusa kwako, nadhani ujumbe umeshafika. (Kicheko)

SPIKA: Subiri na wewe umeweka historia, kwa hiyo, nimekuruhusu toa salamu zako. (Kicheko)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, sasa naomba nijibu swali la Mheshimiwa Zainab Katimba kuwa ni kweli anayoyasema Mheshimiwa Zainab Katimba na ndiyo maana nataka nikiri mbele ya Bunge lako, wakati wa mijadala mingi inayoendelea juu ya masuala mazima ya ajira na utumishi, jambo la mazoezi ya kujitolea au mafunzo ya vitendo limekuwa ni moja ya jambo la mjadala mkubwa.

Mheshimiwa Spika, Bunge lako limesema kwa sauti kubwa na Serikali imesikia. Ndiyo maana sasa tuko katika mchakato wa kufanya review ya Sheria yetu ya Utumishi wa Umma ili kuweza kuangalia mapungufu yote yaliyopo na kama nilivyosema kwenye ahadi yetu kwamba tutakapokuwa tayari tutaileta hapa na Bunge lako litapata nafasi ya kutoa mawazo na sisi kama Serikali tuweze sasa kutengeneza sheria ambayo itakuwa inabadilisha Sheria ya Utumishi wa Umma ili kuweza kutengeneza mustakabali mzima wa ajira na vipaumbele katika nchi yetu.