Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 1

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni muda mrefu sasa wastaafu hawa tokea waliostaafu kipindi cha miaka ya 2020 hadi 2021. Ni bajeti gani ambayo imepanga fedha hizo kupewa wastaafu hawa. Ahsante. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kama nilivyosema, wastaafu jumla walikuwa 624, ili kulipa madeni haya lazima kufanaya uhakiki. Kama nilivyosema, tumeshahahikiki tayari wastaafu 579 ambao ndiyo jumla ya fedha hizo ambazo zimepangwa katika mwaka wa fedha kulipwa, ambazo ni shilingi 806,067,788.02. Hao wengine waliobakia nao tunaendelea na uhakiki ili kujiridhisha kwamba tunalipa stahiki zao bila kumpunja mstaafu yeyote katika Jeshi la Polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali inahakikisha itatenga hizi fedha ili kuwalipa baada ya uhakiki huu kukamilika. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na fedha za wastaafu lakini kumekuwa na changamoto kubwa kwa watumishi wanaofanya kwenye Wizara hiyo, wanapohama kutokulipwa madai yao ya uhamisho kwa wakati.

Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha inawalipa kwa haraka? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni kweli moja ya changamoto zinazotokea pale kunapokuwa na uhamisho ambao haukuwepo kwenye bajeti kwa mwaka husika. Nakuhakikishia kwamba, uhamisho wote ambao umefuata taratibu kamili, wote watalipwa na hasa hii inatakiwa baada ya kuhakiki gharama hizo na kuingiza kwenye bajeti ya mwaka husika, watumishi hawa wanaohama wanalipwa stahiki zao kama ambavyo wamestahili. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 3

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itakuja kumaliza migogoro iliyopo kati ya Gereza ya Urambo na wananchi wanaozunguka gereza hilo ambapo migogoro imedumu kwa muda mrefu? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hili lije kama swali au kama atataka takwimu tutampa.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 4

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tunajua mtumishi kabla hajastaafu ana miezi sita ya kumwandaa kustaafu. Je, ni nini sasa tamko la Serikali kuandaa mapema hayo malipo ya kusafirisha mizigo ya wastaafu ili wasiendelee kunyanyasika kama ilivyo sasa hivi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kama nilivyosema mwanzo ni kweli moja ya changamoto ambazo huwa zinakuwepo ni kwa wale ambao wanastaafu lakini bado kwenye bajeti yetu hatujaweka. Kwa sababu, ni kweli kwamba wanaostaafu wanajulikana, dhamira ya Serikali yetu ni kuhakikisha wote wanalipwa kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunahakikisha kila unapotokea mwaka husika ambao wanaastafu wanawekwa kwenye bajeti za Serikali ili kulipwa kwa wakati bila kufanya ucheleweshwaji wowote kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 5

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la watu wanaostaafu kuchelewa kulipwa mizigo ni kubwa, hata kwenye Ripoti za CAG ipo na tatizo la uhamisho na lenyewe ni kubwa. Kwa Mkoa wa Mara, kuna watu ambao hawajalipwa huu ni mwaka wa tatu mpaka wa nne mfululizo ikiwemo na Wilaya ya Bunda.

Je, ni lini Serikali mtalipa madeni ya mizigo na uhamisho kwa waataafu wa Mkoa wa Mara? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ninaomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali ina dhamira njema ya kuhakikisha wastaafu wanalipwa stahili zao kwa wakati, ikiwemo usafirishaji wa mizigo na mafao yao ya kustaafu. Kwa hiyo, moja ya maeneo ambayo tunaweka msisitizo ni kuhakikisha kila mwaka wa bajeti tunaweka bajeti ya kutosha ili kufidia madeni ya nyuma. Pili, kuhakikisha wale wanaostaafu katika mwaka husika wanalipwa kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba, Serikali itaendelea kuwalipa kwa wakati kadri ambavyo fedha zitapatikana katika bajeti ya kila mwaka. Nakushukuru sana.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza: - Je, lini Serikali italipa madeni ya fedha za kusafirishia mizigo kwa Askari Wastaafu?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kutokana na changamoto ambayo imeendelea kujitokeza kwa Askari wetu wanapostaafu kucheleweshewa mafao yao, kwanini Serikali sasa isije na mpango wa kufanya uhakiki angalau mwaka mmoja kabla ili mtumishi au askari anapostaafu apate mafao yake pamoja na fedha za usafiri? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Sisi tunalichukua hili na ni maeneo ambayo tunayafanyia kazi kama nilivyosema kuhakiki mapema. Mosi, madeni na Pili, mahitaji ya mwaka husika ili kupunguza ucheleweshaji huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali tunalifanyia kazi hili kama ambavyo wamesema na tunahakikisha tunafanya hivyo ili kupunguza adha kwa wastaafu hawa katika maeneo yote. Nakushukuru sana. (Makofi)