Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niishukuru Serikali kwa maamuzi hayo mazuri na jibu zuri ambalo wameweza kutujibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati barabara hii inapanuliwa kuna wananchi ambao walikuwa wamejenga pale na walibomoa nyumba zile ili kupisha ujenzi wa barabara ile; je, ni lini watapata fidia yao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; naishukuru Serikali kwa sababu imeleta taa za barabarani katika barabara hii ya Kenya Road. Lakini taa hizi zimewekwa kwa mbali sana kiasi kwamba hazimuliki vizuri.

Ni lini sasa zile sehemu ambazo hazina taa za barabani zikiwemo za Masara, barabara ya Musoma pamoja na Magena watawekewa taa za barabarani? Ahsante. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Michael Mwita Kembaki, Mbunge wa Tarime Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la fidia kwa wale waliobomolewa kupisha ujenzi wa barabara hii ni kweli kwamba wale wote waliobomolewa ni kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1967 na marekebisho yake ya mwaka 2007 Na. 13, kwamba waliokuwa ndani ya hifadhi ya barabara kwa maana ya mita 22.5, hawa ndio walioguswa, lakini waliokuwa nje ya hifadhi ya barabara, mpaka mita 30 hawakuguswa. Kwa hiyo hapa hakutakuwa na fidia kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa suala la taa za barabarani; tumewaelekeza managers wote wa TANROADS nchi nzima kwamba lazima watenge fedha kwa ajili ya kuweka bajeti za taa barabarani na kwa maana hiyo kwenye mwaka wa fedha ujao katika eneo hili la Tarime Mjini, tumetenga shilingi milioni 270 kwa ajili ya kusimika taa za barabani na mitaa yake yote. Na hata hivyo, kuna taa nyingine ambazo zimeshasimikwa lakini tutaongeza zaidi ili huu mji uweze kupendeza zaidi, ahsante.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; kwa nini ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Magole – Turiani – Mziha – Handeni umeanzia Magole na kuishia Turiani na kuacha kipande cha Handeni – Mziha – Turiani?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kwagilwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii aliyoitamka kwamba imeanzia sehemu hiyo kipande na kingine kimeachwa, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango wa Serikali ni kujenga yote. Kwa hiyo tumeanza hicho kipande, lakini hata kipande kingine pia tutakimalizia, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali ina mpango gani sasa wa kuweka taa za barabani katika Mji wa Nyamilangano ambao tayari umewekewa kilometa tatu za lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, taa za barabarani katika maeneo ambayo ameyasema tumetenga kwenye bajeti ambayo imepitishwa na Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo tutamuwekea katika eneo lake Mheshimiwa Mbunge.

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa kampeni za Rais wa Awamu ya Tano, aliahidi katika Mkoa wa Shinyanga atatujengea barabara kilometa 10, na juzi, mapema mwaka huu, Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Mpango, aliahidi wakati akizindua Hospitali ya Rufaa ya Mwawanza pale Shinyanga, kwamba atatujegea kilometa 10.

Nini mpango wa Serikali kuhakikisha inatekeleza ahadi hizo za viongozi wa Kitaifa, hasa katika mwaka huu wa fedha? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salome Makamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi zote za viongozi wa Kitaifa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi katika bajeti ya mwaka huu tumezizingatia kwa kiwango kikubwa. Na kwa maana hiyo, hata barabara aliyoisema Mheshimiwa Salome Makamba ni miongoni mwa barabara ambazo tunakwenda kuzijenga, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kuanzia Kalela – Munzeze mpaka Buhingwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitamka kuanza Kalela na kuendelea ni barabara ambayo katika bajeti ya mwaka ujao tumeitengea fedha kwa ajili ya kufanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: - Je, kwa nini ujenzi wa barabara ya Tarime – Nyamwaga – Serengeti umeanzia katikati badala ya kuanzia Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lupembe, barabara ya kutoka Kibena – Lupembe – Madeke hadi Taveta, Mheshimiwa Swalle, Mbunge huyu, amekuwa akiizungumza sana barabara hii. Ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa kwa lami ili wananchi wa Lupembe wapate imani na Serikali yao?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara hii inaunganisha Mikoa ya Njombe, Iringa na inakwenda mpaka Morogoro, na katika mwaka wa fedha huu ambao tutaanza, ni miongoni mwa barabara ambazo tumezitengea fedha, ahsante.