Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya za Liwale, Nachingwea, Ruangwa na Lindi Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; je, ni lini Serikali itatoa pesa au kutenga pesa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA Kilwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; vifaa vilivyopo kwenye Chuo cha VETA Lindi Mjini ni vya kizamani sana; je, Serikali haioni haja ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya Lindi Mjini? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha jibu kwenye majibu yangu ya swali la msingi kwamba vyuo hivi vinajengwa katika Wilaya 64, na Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa Wilaya 64 ambazo zinajengewa, na tayari tumeshapeleka shilingi milioni 228 kule Kilwa, na usimamizi wa chuo kile kinachojengwa pale unafanywa chini cha Chuo chetu cha FDC ambacho kipo katika Wilaya hiyo ya Kilwa.

Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, lakini niwaondoe hofu wananchi wa Kilwa, hata pale Kilwa napo ni miongoni mwa Wilaya 64 ambazo zinajengewa vyuo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la pili, amezungumza suala la vifaa; ni kweli tukiri kwanza katika vyuo vyetu vya zamani tulikuwa na vyuo 45 vya zamani ikiwemo na hiki cha Lindi, lakini tumpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa utashi wake na maono yake, katika kipindi hiki kifupi tumeweza kukamilisha vyuo 29 na hivi sasa tunakwenda kujenga vyuo vingine 65, vyuo 64 katika Wilaya na kimoja cha Mkoa. Hivi sasa Serikali inafanya tathmini kwa vyuo vile vyote 45 vya zamani na hivi 29 ambavyo tulijenga katika mwaka uliopita wa fedha, tathmini ya vifaa pamoja na mitambo mbalimbali kwa ajili ya kujifunzia na kufundishia. Kwa hiyo, tuko njiani kupeleka vifaa hivyo.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Vyuo vya VETA katika Wilaya za Liwale, Nachingwea, Ruangwa na Lindi Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Swali langu ni hili; je, Serikali inaweza ikatoa kauli gani kuhusu uwezekano wa kuingia ubia na taasisi za kidini ambazo zilijenga Vyuo vya Ufundi Stadi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimtoe hofu Mheshimiwa Kimei, utaratibu huo upo. Naomba tu kwa vile ni suala mahususi, baada ya kikao chetu hiki au baada ya kipindi hiki cha maswali, tunaweza tukakutana ili tuweze kuangalia hilo eneo au hivyo vyuo ulivyovitaja namna gani tunaweza tukatengeneza huo ushirikiano wa kutoa mafunzo kwa pamoja baina ya wawekezaji pamoja na Serikali, nakushukuru sana.