Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, lini Kata za Miyombweni, Malilo, Songwe na Luhanga zitawekwa anuani za makazi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, baadhi ya maeneo yale wamesharudishiwa wananchi kwa matumizi yao. Sasa ni lini Serikali itayaratibu na kuyapanga upya maeneo yale kwa maana ya vijiji, vitongoji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ikitokea wananchi wamechoka jina la mtaa, je, wanaweza wakabadilisha jina? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali la kwanza; eneo ambalo limerudishwa katika vijiji tutashirikiana kwa sababu yanagusa Wizara mbalimbali, tutashirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, tutashirikiana na Wizara ya Ardhi, lakini vilevile tutashirikiana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ili kuona jinsi ya kulifanyia kazi na pale ambapo tutajiridhisha kwamba limesharejeshwa kweli, basi anuani za makazi zitawekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa pili, swali la pili, pale ambapo wananchi au Serikali inataka kubadilisha jina la mtaa au jina la barabara; kuna utaratibu ambao unapitiwa. Lazima vikao vifanyike kwa ngazi ya chini na wananchi washirikishwe na pale ambapo Serikali itajiridhisha kwamba ndani ya kata moja kuna jina la mtaa linalofanana na mtaa mwingine basi Serikali itawashirikisha wananchi ili kubadilisha, lakini hata pale ambapo wananchi wanalalamika katika maeneo hayo yote hayo yatafanywa kulingana na utaratibu uliowekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna kesi iko pale Goba, kwenye utaratibu ambao walishirikishwa mwanzoni waliamua kwamba jina lao liitwe Maghorofani, lakini baada ya kuwa wanatumia ile anuani wakajikuta kwamba jina lile linaitwa Janguo. Sasa tumeshatuma timu yetu kwenda kuhakikisha kwamba ni nani mefanya ujanja huo wa kubadilisha jina la mtaa bila wananchi wenyewe kujua kwamba utaratibu upi umetumika katika kubadilisha hilo jina.