Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatafuta suluhisho la kudumu la kudhibiti wanyama waharibifu wa mazao na ugonjwa wa mnyauko?

Supplementary Question 1

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali katika eneo ambalo imeongelea la kudhibiti kweleakwelea, viwavijeshi, nzige na wanyama wengine waharibifu, lakini katika eneo hilo suala la ngedere ni ngumu sana kulidhibiti kwa aina ya kupitia kilimo anga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Wilaya ya Missenyi imekuwa ni janga kubwa na sisi kama wananchi kupitia juhudi za Mbunge na Waheshimiwa Madiwani tulitafuta suluhisho la kununua dawa aina ya carbofuran ambayo inaua ngedere hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua mchango wa Waheshimiwa Madiwani na Mbunge kununua dawa hiyo; je, Serikali haioni kuna haja ya ku–support juhudi hizo kuchangia hizo fedha au kuelekeza Halmashauri ikatenga bajeti kwa ajili ya kununua dawa hiyo ili wananchi sasa wakilima waweze kuvuna?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Tunajua Serikali imefanya kazi kubwa katika kupambana na suala la mnyauko, lakini mpaka sasa hivi bado unaleta usumbufu katika maeneo yetu.

Je, ni hatua gani ambayo Serikali imefikia katika kufanya utafiti ili sasa tuweze kupata suluhisho la kudumu la ugonjwa wa mnyauko? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili la kwanza la kuhusu dawa ambayo inatumika pale Missenyi nataka nichukue fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya waende kuangalia dawa hiyo ambayo inatumika, na kama ina ufanisi sisi kama Serikali pia, tutaunga mkono kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu mkakati wa kudumu; kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, moja kati ya kazi kubwa ambayo tunaendelea kuifanya hivi sasa ni kuhakikisha kwanza kabisa tunang’oa na kuchoma moto mashina yale yote ambayo yalikuwa yana ugonjwa wa mnyauko ili ugonywa huu usisambae, lakini la pili, tunawajengea uwezo Kituo chetu cha Utafiti wa Kilimo cha TARI - Maruku, ili waweze kufanya utafiti na badae kuzalisha miche bora ambayo itakuwa na ukinzani na ugonjwa huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka ujao wa fedha tumetenga shilingi milioni 800; shilingi milioni 400 inakwenda kwa ajili ya utafiti na uzalishaji wa miche bora ya migomba. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatafuta suluhisho la kudumu la kudhibiti wanyama waharibifu wa mazao na ugonjwa wa mnyauko?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itakuja na mkakati wa uzalishaji miche kwa kutumia teknolojia ya chupa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 zimetengwa shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuwajengea uwezo TARI – Maruku ili waweze kuanza teknolojia mpya ya uzalishaji wa miche safi kupitia tissue culture ambayo itasaidia sana katika kutatua changamoto hii ya ugonjwa wa mnyauko.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itatafuta suluhisho la kudumu la kudhibiti wanyama waharibifu wa mazao na ugonjwa wa mnyauko?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la kitunguu linalolimwa sana Wilayani Kilolo limekumbwa na ugonjwa unaoitwa kaukau kwa lugha ya mtaani ambao haujulikani na vitunguu vinakauka mara tu vinapokuwa vimepandwa.

Je, Serikali iko tayari kutuma wataalamu ili kufanya uchunguzi na kutafuta suluhisho katika ugonjwa huu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa taarifa hii, Jumatatu wataalam kutoka Wizara ya Kilimo watakuwepo jimboni kwake kwa ajili ya kushughulikia tatizo hilo. (Makofi)