Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. ALEKSIA A. KAMGUNA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje kukomesha uvuvi haramu wa kuvua samaki kwa kutumia nyavu zenye matundu madogo?

Supplementary Question 1

MHE. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema kuwa wawekezaji kuingiza hizi nyavu zilizo bora wanahamasisha; je, kuna mkakati gani wa Serikali wa kuhamasisha hawa wawekezaji wanaoleta hizi nyavu badala ya kuleta wakaanzisha viwanda hapa Tanzania vya kutengeneza hizi nyavu zinazotakiwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mto Kilombero kuna wavuvi wanaovua sana sana kutoka Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi; je, kuna mpango gani wa kuhamasisha na kuwapatia nyavu bora za uvuvi? Ahsante sana.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Morogoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, je tumejipangaje kwenye kuhamasisha juu ya ujenzi wa viwanda vya nyavu hapa nchini? Jambo hili tayari linafanywa na tumekwisha kuanza kupata viwanda ambavyo vinatengeneza nyavu. Pale Mwanza tunacho kiwanda kipya kinaitwa Ziwa Net ambacho kinatengeneza nyavu na kuwauzia wavuvi na tunayo maombi pia vilevile ambayo tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa ajili ya uwekezaji kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ni suala la zana kwa ajili ya wavuvi kwenye mto Kilombero. Jambo hili nimelichukua kama ombi la Mheshimiwa Mbunge, Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum na nitakwenda kuzungumza naye ili kuweza kuandaa wavuvi wa Mto Kilombero katika vikundi na baadae na wao ikiwezekana waweze kupata hizi zana kama ambavyo wanapata wavuvi wengine nchini.