Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID K.n.y. MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya uhakiki ili kuwarejesha walengwa 2,500 waliosimamishwa kupokea ruzuku ya TASAF?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID ABDALLA RASHID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba uhakiki umefanyika na wananchi hao wamesharejeshwa, lakini ni lini sasa watapatiwa malimbikizo yao ya ruzuku kutoka pale ambapo walisimamishwa na ukizingatia kwamba hasa hawa ambao walisimamishwa ni wanawake?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna makundi mawili; la kwanza ni wale ambao baada ya uhakiki walionekana wamekosa sifa na hawa ni 2,500 lakini wako ambao walipokosa sifa walikata rufaa wakarejeshwa, tutaangalia uwezekano wa kuanzia pale walipokuwa wamesimama au taratibu zinatakaje ili waweze kulipwa au wataendelea kuanzia hapa ambapo wamekuwa cleared.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili ni jambo la kulifanyia kazi, tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge muuliza swali Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi ili atuambie hasa ni wapi, lakini kimsingi Serikali ili wapembua kwa makundi hayo mawili na uamuzi huo ndio ulikuwa umefikiwa mpaka hatua za mwisho.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID K.n.y. MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya uhakiki ili kuwarejesha walengwa 2,500 waliosimamishwa kupokea ruzuku ya TASAF?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kati ya waliopata sifa ni pamoja na wanawake na kaya nyinginezo za Mkoa wa Kilimanjaro ambao walipewa sasa ajira za muda, lakini baada ya kufanya ajira hizo vizuri hawajalipwa kwa vipindi viwili sasa.

Je, ni lini, Serikali itatoa malipo hayo ili malalamiko yaondoke katika mioyo yao?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyomgeza la Mheshimiwa Shally Raymond kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii ni taarifa na nimeisikia sasa kutoka kwake kwamba Mkoa wa Kilimanjarpo kuna wale ambao waliofanya kazi za TASAF za miradi ya kipindi maalumu na kwamba bado hawajalipwa basi acha tukalifanyie kazi halafu tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge.