Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsanste na nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; katika Wilaya ya Meatu kuna vituo vya afya ambavyo vimefunguliwa viwili Iramba Ndogo pamoja na Mwasengela. Iramba ndogo ina wafanyakazi watatu; mmoja ni mganga na wawili ni wauguzi, kwa hiyo hawatoshi kabisa, lakini katika Kituo cha Afya cha Mwasengela chenyewe hakina kabisa watumishi wa afya na kinategemewa kufunguliwa tarehe 1 Julai; naomba majibu ya Serikali kuhusu wafanyakazi katika vituo hivi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili liko katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa; Hospitali ya Maswa ni kubwa sana lakini watumishi hawatoshi, naomba nipate jibu la uhakika kwamba ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Minza, la kwanza la Iramba Ndogo kupata watumishi wa ziada na Mwasengela; niseme tu kama nilivyokwishakutoa maelezo kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali inaajiri watumishi wa afya 8,070 na katika hawa tutapanga kwanza kwenye maeneo yale yenye upungufu mkubwa ikiwemo Iramba Ndogo, lakini vilevile kwa sababu kituo hiki cha Mwasengela ni kituo kipya ambacho kinaenda kufunguliwa tarehe 1 Julai na kama sikosei kipo Kisesa, tutahakikisha hizi ajira mpya kwa sababu wataingia kazini mwaka huu wa fedha ambao tunautekeleza sasa na tarehe 1 Julai ni mwaka ule mwingine wa fedha, tayari kituo hichi kinapofunguliwa watumishi hawa wa afya watakuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda tu kwenye hili alilogusia la Hospitali ya Wilaya ya Maswa vilevile kwenye hizi ajira tutapeleka maeneo ambayo yana upungufu mkubwa ikiwemo Hospitali ya Wilaya ya Maswa. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na ukubwa wa jiografia wa Wilaya ya Hanang; je, ni lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya pamoja na vituo vya afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halamga kuhusu Hanang na vituo vya afya, zahanati, hospitali ya wilaya na vituo vya afya ambavyo vina upungufu wa watumishi, kama nilivyokwishakusema kwenye majibu yangu ya msingi katika ajira hizi zilizotangazwa na Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu ajira 8,070 nitahakikisha pia Hanang wanapata watumishi wa afya.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 3

MHE: DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la watumishi linaendana na vifaa tiba. Njombe tuna vituo vya afya viwili vimejegwa kwa nguvu za wananchi na mapato ya ndani. Watumishi wameshapelekwa tunashukuru Serikali, lakini watumishi hao sasa ni kama hawana kazi kwa sababu vifaa tiba havijapelekwa.

Sasa swali langu, Serikali haioni ni busara kuhakikisha kwamba pale ambapo watumishi wamepelekwa, lakini vifaa tiba havijaenda basi wakafanya haraka kupeleka vifaa tiba ili watumishi hao sasa wafanye kazi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwanyika la vifaa tiba, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza sana wananchi wa Jimbo la Njombe kwa kujenga kwa nguvu zao wenyewe vituo hivi vya afya na vilevile Halmashauri ya Mji kwa kujenga pia kwa kupitia mapato yao ya ndani na hili ndio tunatamani kuliona kila Halmashauri ikitenga fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya kusaidia wananchi katika sekta ya afya na sekta ya elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa suala la vifaa tiba ni kipaumbele cha Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha vifaa tiba vya kisasa vinakwenda katika maeneo yote nchini ikiwemo kule Wilayani Njombe na tutakaa na Mheshimiwa Mbunge na kuangalia kwenye bajeti iliyotengwa ni kiasi gani kimetengwa kwa jaili ya vifaa tiba na hiyo fedha iliyokuwepo basi vifaa tiba hivyo viweze kupataikana mara moja.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Kata ya Soya, Wilaya ya Chemba tulijengewa na wafadhili, kuna baadhi ya vifaa tiba vipo na baadhi havipo ikiwemo x–ray machine, lakini na watumishi mpaka leo kituo kimekamilika tangu mwaka jana. Hivyo vifaa tiba havijakamilika na watumishi hatuna kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itatupelekea vifaa tiba pamoja na watumishi ili hospitali kwa maana ya kituo cha afya hicho kiweze kufanyaa kazi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kituo cha Afya cha Kata ya Soya, Wilayani Chemba Serikali itapeleka watumishi, katika hawa watumishi wanaoajiriwa kama nilivyokwisha sema katika majibu yangu ya msingi na kwenye vifaa tiba tutaangalia kwenye bajeti iliyotengwa ni kiasi gani inatakiwa kwa ajili ya kwenda kununua hivi vifaa kama x–ray na vinginevyo basi Serikali iweze kupeleka fedha hizo na vifaa hivi viweze kununuliwa na wananchi wa Soya waweze kupata huduma hii.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wimbi kubwa la kuhama watumishi kwenye Idara ya Afya kwenye Halmashauri hasa zile za pembezoni. Mfano Liwale tulipata watumishi 80 lakini watumishi wale leo ukienda kuwahesabu hata 15 hawafiki, wanahama 36 wanahamia wawili; je, Serikali ina mpango gani kudhibiti huo uhamaji wa watumishi holela?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, suala ambalo ananiuliza Mheshimiwa Kuchauka Serikali imelitambua na tayari tunaweka mikakati hasa kwenye ajira hizi ambazo wanaingia kazini muda siyo mrefu, kuona tutaweka mikakati ambayo itadhibiti hili la watu kuhama. Lakini pia nichukue nafasi hii kuwaeleza Wakurugenzi wa Halmashauri ambao ndio waajiri katika maeneo haya wahakikishe hawapitishi barua za watumishi ambao hawajathibitishwa kazini. Mtumishi anatakiwa walau akae miaka mitatu katika kituo chake kipya cha ajira, kwa hiyo, wafuate taratibu hizi, wasipitishe barua hizi ili watumishi hawa maana yake wameajiriwa kwenda kujaza upungufu ule ambao upo katika maeneo hayo. Sasa wanapopitisha barua hizi ili hawa wahame tayari wanazidisha upungufu katika maeneo haya.

Kwa hiyo, niliona nichukue muda kulizungumzia hili hapa ndani ili Wakurugenzi wetu wa Halmashauri ambao ni waajiri waweze kuelewa kufuata taratibu hizi za kiutumishi.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 6

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, je, Serikali haioni haja ya kuweka kipaumbele kuongeza watumishi wa afya kwenye Halmashauri mpya ikiwepo Halmashauri ya Mji wa Nanyamba pamoja na Newala Vijijijni? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la Mheshimiwa Hokororo, ni kweli tunaona haja ya kuongeza watumishi hasa katika Halmashauri hizi mpya kama ya Nanyamba na ndiyo maana Serikali ilitenga bajeti katika mwaka huu wa fedha kuajiri watumishi 21,390 nchi nzima katika sekta ya elimu na afya, kwa ajili ya kupeleka katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kama Halmashauri ya Nanyamba.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 7

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana Naibu Waziri wa Afya alitembelea Zahanati ya Kata ya Lemooti, Kijiji cha Lemooti, Wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha na kuwaahidi kuwa Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya kumalizia miundombinu.

Je, ni lini sasa pesa hizo zitaenda ili kina mama wapate huduma ya uhakika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kupeleka fedha katika Zahanati hii ya Lemooti kule Wilayani Monduli, tutaangalia katika bajeti ambayo imepitishwa na Bunge lako tukufu ya mwaka 2023/2024 kuona ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi au ukarabati wa zahanati katika Wilaya ya Monduli ili iweze kuelekezwa katika Zahanati hii ya Lemooti na kama haikutengewa fedha, basi tutaangalia katika mwaka wa fedha 2024/2025 zahanati hii iweze kutengewa fedha.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza watumishi wa afya katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 8

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pamoja na majibu yake mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri juu ya watumishi na mikakati ambayo ataiweka. Sasa swali langu ni kwamba je, mkakati gani wa ziada utakaouweka hasa kwa Mkoa wa Lindi kwa sababu suala la uhamaji wa watumishi ni kubwa sana? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, Mbunge wa Mchinga ni kama ambavyo nimetoa maelezo wakati namjibu Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale ambao wote wanatoka Mkoa wa Lindi na kweli Waheshimiwa Wabunge hawa wamekuwa wakilifuatilia sana suala hili Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikisha Mkoa wao unapata watumishi wa kutosha na watabaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati ambao tumeuweka ni wa kuhakikisha wale wote walioomba ajira hizi, watambue kwanza tutawafahamisha wanapochukua barua zao za ajira kwamba ajira hizi ni zimekwenda kujaza nafasi katika maeneo yenye upungufu mkubwa hapa nchini wa watumishi ili wahudumie Watanzania ikiwemo Mkoa wa Lindi. Hivyo basi itakuwa ni lazima atumikie nafasi hiyo katika eneo hilo ule muda ambao anatakiwa awe katika mtazamio (probation period) wa mwaka mmoja na baada ya hapo bado hatohama walau kwa miaka mingine miwili ina maana jumla inakuwa ni miaka mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nirudie tena hapa kusema na kuongea na Wakurugenzi kupitia Bunge lako tukufu hili, wasipitishe barua ya mtumishi yeyote ambaye ni ajira mpya kwa sababu wakati anaomba ajira hiyo alitambua Serikali inafanya kazi kila pembe ya nchi yetu, na kwamba unapoomba kazi hiyo utapangiwa kwenda kuwatumikia Watanzania mahali popote nchini hapa. Kwa hiyo, wanapopewa barua za ajira waende wakatumikie Watanzania katika maeneo hayo.