Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa DMDP Awamu ya Pili utaanza kwa lengo la kutatua changamoto ya miundombinu Kigamboni?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwanza nipongeze sana majibu ya Serikali na nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais na Mawaziri wa Fedha, TAMISEMI na Ujenzi kwa kuendelea kuchakata jambo hili liende vizuri katika mchakato huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja tu la nyongeza; kwa sababu Serikali ipo katika hatua za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina maana yake tayari imeshafanya utambuzi wa barabara zote zitakazoingia kwenye mradi wa DMDP Awamu ya Pili.

Je, ni barabara zipi ndani ya Jimbo la Kibamba ambazo na zenyewe zitakuwa sehemu ya mradi huu DMDP Awamu ya Pili?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, namna mradi huu ulivyokuwa design kwamba kila Halmashauri katika Mkoa wa Dar es Salaam imewasilisha mapendekezo ya barabara ambazo zitatakiwa kufanyiwa ukarabati kupitia mradi huu wa DMDP II.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumjulisha Mheshimiwa Mtemvu na Wabunge wote wa Dar es Salaam kwamba kwa maelekezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mheshimiwa Anjela Kairuki wiki ijayo mtaitwa wote Waheshimiwa Wabunge wa Jiji la Dar es Salaam ili kushuhudia utiaji saini wa mradi huu wa consultancy ambazo anaenda ku-design barabara zetu hizi. Kwa hiyo, nimtoe hofu ni barabara zote kama walivyoziwalisha wao katika halmashauri zao ambazo zitawekwa katika mradi huu.