Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha pesheni za wastaafu zinalipwa kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza niseme kabisa Mheshimiwa Waziri sijaridhishwa na majibu haya, hii takwimu uliyoionesha hapa kwamba bado wastaafu 1,780 hawajalipwa lakini niende kwenye maswali mawili labda nitaridhika.

Sasa Mheshimiwa Waziri mnawatambuaje wastaafu ambao walistaafu miaka mingi wakahamia wengine vijijini, hawako kwenye mifumo hii ya kieletroniki na umesema wanafanyiwa uhakiki kuwatambua kupitia akaunti zao tayari wengine walishafungiwa na akaunti?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; hauoni ni kumweka mtu kwenye mazingira magumu sana ambaye anaitumikia Serikali wakati wake unapofika wa kustaafu halafu zinaanza chenga za kumlipa mafao yake.

Je, ungekuwa ni wewe ukamaliza Ubunge wako halafu mafao yasipatikane ungefikiriaje Mheshimiwa Waziri? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nicodemus Henry Maganga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza awali na anasema hajaridhika na majibu, lakini takwimu sahihi za Serikali chini ya mifuko na hizo kwamba wastaafu ambao wanalipwa ni hao 186,605 na kama ana takwimu tofauti basi tunamkaribisha ili tuweze kuangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili kuhusiana na suala la wastaafu ambao wako vijijini anasema masuala ya mtandao na kadhalika. Hao wanaendelea kuhudumiwa, katika ofisi zetu zote za mifuko na wanachama wale wamefunguliwa na hawa niliowataja wote wana akaunti hizo za benki na bado kuna desk ambalo linawahudumia wastaafu wetu na tumeajiri watu maalum kabisa wa kutoa huduma hiyo kwa wateja wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kama ana jambo mahususi haliwezi kuwa la watu wote ni la hao watu wachache ambao anawasema na kama wapo anifikishie ili niweze kuchukua hatua zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ni kuhusiana na kwamba ucheleweshaji wa ulipaji wa mafao, imebaki kuwa historia, tumeshafanya mabadiliko sasa hivi tunalipa kieletroniki na kuhusiana na mafao kama ni ulipaji kila mwezi kabla ya tarehe 25 tunalipa fedha hizo. Kwa hiyo, hilo ni suala la kihisroria analolielezea sasa hivi tumefanya mabadiliko makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii pia kuwaagiza Wakurugenzi na Mameneja wote wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii katika Mikoa waendelee kusimamia na kufanya lile suala la compliance kufatilia michango ya wanachama, lakini pili kuendelea kuhakikisha kwamba hakuna mstaafu yoyote ambaye anapata shida katika kipindi hiki, ahsante. (Makofi)